عن ابن عباس رضي الله عنهما أنه رأى رجلا انْتَفَضَ لما سمع حديثا عن النبي صلى الله عليه وسلم في الصفات -استنكارا لذلك– فقال: "ما فَرَقُ هؤلاء؟ يجدون رِقَّةً عند مُحْكَمِهِ، ويَهْلِكُونَ عند مُتَشَابِهِهِ" .
[صحيح] - [رواه عبد الرزاق وابن أبي عاصم]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Abbasi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- yakwamba yeye alimuona mtu alishituka aliposikia mazungumzo kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika sifa (za Allah) -akafanya kama ishara ya kulipinga hilo- akasema: "Ni nini kinachowaogopesha hawa? wanapatwa na ulaini (wanazikubali) aya zilizo wazi, na wanaangamia katika aya zinazotatiza".
Sahihi - Imepokelewa naIbn Abii A'swim

Ufafanuzi

Anawakemea bin Abbasi watu miongoni mwa wale waliohudhuria kikao chake katika watu wa kawaida wanaopatwa na hofu pale wanaposikia chochote katika hadithi za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kuhusu sifa, na wanatikisika kama ishara ya kulipinga hilo, haijapatikana kwao imani ya wajibu kwa yale yaliyothibiti toka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na wakajua maana yake kutoka ndani ya Qur'ani ambayo muumini hawezi kuwa na shaka, na baadhi yao huzichukulia katika maana isiyokuwa yake aliyoitaka Mwenyezi Mungu wakaangamia kwa hilo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama
Ziada