عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «ما مِنْ يومٍ يُصْبِحُ العِبادُ فيهِ إلا مَلَكَانِ يَنْزِلَانِ، فيقولُ أَحَدُهُمَا: اللهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا، ويقولُ الآخَرُ: اللهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakuna siku ambayo wanaamka ndani yake waja isipokuwa kuna Malaika wawili wanateremka, anasema mmoja wao: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mtoaji badala, na anasema mwingine: Ewe Mwenyezi Mungu mpe mzuiaji hasara".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Haipiti siku kwa watu isipokuwa kuna Malaika wawili wanateremka, anasema mmoja wao: Ewe Mwenyezi Mungu mpe atakayetoa katika mali yake kwenye mambo ya kheri kama mambo ya utiifu na juu ya familia na kwa wageni (mpe) badala, duniani na Akhera, na anasema mwingine: Ewe Mwenyezi Mungu muangamize bahili anayezuia yale ambayo Mwenyezi Mungu kamuwajibishia kuyatoa katika mali, muangamize yeye na mali yake.