عن محمود بن لبيد رضي الله عنه مرفوعاً: "أَخْوَفُ ما أخاف عليكم: الشرك الأصغر، فسئل عنه، فقال: الرياء".
[صحيح] - [رواه أحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Mahmudi bin Lubaid- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Ninaloliogopea zaidi kwenu nyinyi: ni shirki ndogo, akaulizwa kuhusu hilo, akasema: ni Riyaa (kujionyesha)".
Sahihi - Imepokelewa na Ahmad

Ufafanuzi

Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa yeye anatuogopea juu yetu, na zaidi analoliogopea juu yetu ni shirki ndogo, na hili ni kwasababu ya yale aliyosifika nayo rehema na Amani zimfikie miongoni mwa ukamilifu wa upole na huruma kwa umma wake, na pupa juu ya yale yanayotengeneza hali zao, na alipojua nguvu ya sababu za shirki ndogo ambayo ni kujionyesha, na wingi wa vishawishi vyake, huenda ikaingia kwa waislamu na hali wao hawajui ikawadhuru; hivyo akawatahadharisha nayo na akawaonya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa riyaa (kujionyesha) kunaogopeka zaidi kwa watu wema kuliko fitina ya masihi dajali.
  2. Kutahadhari na kujionyesha na ushirikina kwa ujumla.
  3. Huruma yake kubwa rehema na Amani zimfikie juu ya umma wake na pupa yake ya kutaka waongoke, na kuwanasihi kwake.
  4. Nikuwa shirki inagawanyika katika shirki ndogo na kubwa- Shirki kubwa ni mtu kumsawazisha asiyekuwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu katika yale ambayo ni maalumu kwa Mwenyezi Mungu, na shirki ndogo ni yale yaliyokuja katika ushahidi kuwa ni shirki na yakawa hayajafikia katika kiwango cha ukubwa: Na tofauti kati yake: (a) Shirki kubwa inaporomosha matendo yote, na shirki ndogo inaporomosha jambo ililoambatana nayo (b) Nikuwa shirki kubwa inamuweka mfanyaji wake motoni milele, na shirki ndogo haipelekei kuishi motoni milele (c) nikuwa shirki kubwa inamtoa katika uislamu, na ndogo haimtoi katika uislamu.