عن محمود بن لبيد رضي الله عنه مرفوعاً: "أَخْوَفُ ما أخاف عليكم: الشرك الأصغر، فسئل عنه، فقال: الرياء".
[صحيح] - [رواه أحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Mahmudi bin Lubaid- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Ninaloliogopea zaidi kwenu nyinyi: ni shirki ndogo, akaulizwa kuhusu hilo, akasema: ni Riyaa (kujionyesha)".
Sahihi - Imepokelewa na Ahmad
Anatueleza Mtume rehema na Amani zimfikie katika hadithi hii kuwa yeye anatuogopea juu yetu, na zaidi analoliogopea juu yetu ni shirki ndogo, na hili ni kwasababu ya yale aliyosifika nayo rehema na Amani zimfikie miongoni mwa ukamilifu wa upole na huruma kwa umma wake, na pupa juu ya yale yanayotengeneza hali zao, na alipojua nguvu ya sababu za shirki ndogo ambayo ni kujionyesha, na wingi wa vishawishi vyake, huenda ikaingia kwa waislamu na hali wao hawajui ikawadhuru; hivyo akawatahadharisha nayo na akawaonya.