عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما مرفوعاً: "من حلف بغير الله قد كفر أو أشرك"
[صحيح] - [رواه الترمذي وأبو داود وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Umar- Radhi za Allah ziwe juu yake- akisimulia kutoka kwa Mtume : " Mwenye kumuapia asiyekuwa Allah atakuwa kakufuru au kamshirikisha Allah".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Anatupa habari Mtume- Rehema na amani ziwe juu yake-katika hadithi hii, habari ambayo maana yake ni katazo: kwamba mwenye kukiapia chochote kinyume na Allah,miongoni mwa viumbe, basi atakuwa kakifanya kiumbe hicho alichokiapia kuwa ni mshirika wa Allah ,na atakuwa amekufuru, maana kukiapia kitu inamaana ya kukiadhimisha na kiuhakika utukufu wa kweli ni wa Allah pekee, hivyo asiapiwe asiyekuwa Allah,au sifa miongoni mwa sifa zake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani Pashto Kiassam Albanian
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu nakuwa hilo ni shirki na ni kumkufuru Mwenyezi Mungu.
  2. Nikuwa kutukuza kwa kiapo ni haki ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Hivyo asiape ila kwake.
  3. Nikuwa kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu hakuna uwajibu wa kutoa kafara; kwasababu hakutaja ndani yake kafara, bali kinachomlazimu ni kufanya toba na kuomba msamaha.
  4. Nikuwa kiapo kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni shirki ndogo, na inasemekana kuwa ni shirki kubwa na ukweli nikuwa ni shirki ndogo, wamesema hivyo wanachuoni wengi.