عن عطاء بن يسار وأبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: "اللهم لا تجعل قبري وثنا يُعبد، اشتد غضب الله على قوم اتخذوا قبور أنبيائهم مساجد".
[صحيحان] - [حديث عطاء بن يسار: رواه مالك. حديث أبي هريرة رضي الله عنه: رواه أحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa A'twaa bin Yasari na Abuu Huraira- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Hadithi Marfu'u: "Ewe Mola wangu usilifanye kaburi langu kuwa ni sanamu lenye kuabudiwa, zimekuwa kali hasira za Mwenyezi Mungu juu ya watu walioyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti.
Sahihi - Imepokelewa na Ahmad

Ufafanuzi

Aliogopea rehema na Amani ziwe juu yake kutokea katika umma wake pamoja na kaburi lake yaliyojitokeza kwa Mayahudi na Wakristo pamoja na makaburi ya Manabii wao katika kuchupa mipaka juu yake, mpaka yakawa ni masanamu yenye kuabudiwa, Akamuomba Mola wake asilifanye kaburi lake hivyo, kisha akatahadharisha rehema na Amani zimfikie juu ya sababu iliyopelekea kupata ghadhabu kali na laana kwa Mayahudi na Wakristo, yale waliyoyafanya katika haki za makaburi ya Manabii wao mpaka wakayageuza kuwa masanamu yenye kuabudiwa, wakaingia katika shirki kubwa yenye kwenda kinyume na tauhidi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa kuvuka mpaka katika makaburi ya Manabii kunayafanya kuwa ni masanamu yenye kuabudiwa.
  2. Nikuwa miongoni mwa kuchupa mpaka katika makaburi ni kuyafanya kuwa Misikiti, na hili linapelekea katika ushirikina.
  3. Kuthibitisha kusifika Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Ghadhabu kwa yale yanayoendana na Utukufu wake.
  4. Kuyaendea makaburi kwa lengo la kuyatukuza ni kuyaabudu, na hapo inakuwa ni shirki kwa namna yoyote utakavyokuwa ukaribu wa mwenye kaburi kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  5. Kuharamishwa kujenga misikiti juu ya makaburi.
  6. Kuharamishwa kuswali makaburini hata kama hakujajengwa msikiti.