قول الله تعالى : {فَلا تَجْعَلُوا لِلَّهِ أَنْدَادًا وَأَنْتُمْ تَعْلَمُونَ}. قال ابن عباس في الآية: "الأنداد: هو الشرك، أخفى من دَبِيبِ النمل على صَفَاةٍ سوداء في ظلمة الليل". وهو أن تقول: والله وحياتك يا فلان، وحياتي، وتقول: لولا كُلَيْبَةُ هذا لأتانا اللصوص، ولولا البط في الدار لأتانا اللصوص، وقول الرجل لصاحبه: ما شاء الله وشئت، وقول الرجل: لولا الله وفلان، لا تجعل فيها فلانا؛ هذا كله به شرك".
[صحيح. ملحوظة: لم نجد له حكما للألباني، ولكن قال ابن حجر: (سنده قوي). وقال سليمان آل الشيخ: (وسنده جيد). العجاب في بيان الأسباب (ص 51)، تيسير العزيز الحميد (ص587)] - [رواه ابن أبي حاتم]
المزيــد ...

Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika na hali nyinyi mnajua, Amesema bin Abbas katika aya hii: Washirika, ni ushirikina, uliofichikana kuliko mkanyago wa mdudu chungu katika jiwe kubwa jeusi katika giza nene la usiku". Nayo ni mtu kusema: Namuapa Mwenyezi Mungu na maisha yangu ewe fulani, naapa kwa maisha yangu, na kusema: laiti kisingekuwa kimbwa hiki wezi wangetuvamia, na lau kama si bata huyu wezi wangetujia, na kauli ya mtu kusema kumwambia mwenzie: Akitaka Mwenyezi Mungu na ukitaka wewe, na kauli ya mtu: lau kama si Mwenyezi Mungu na fulani, usimuweke ndani yake fulani hii yote ina ushirikina".
Sahihi - Imepokelewa na Abii Haatim

Ufafanuzi

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika na hali nyinyi mnajua", akawakataza watu wasimfanyie mifano wanaoelekezewa chochote katika ibada zake; na hali wao wanajua kuwa kweli Mwenyezi Mungu yeye pekee ndiye muumbaji na mgawaji wa riziki; nakuwa hawa washirika hawajiwezi bali ni mafakiri (wahitaji) hawamiliki jambo lolote, na ameelezea bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa vijiungu kwa maana ya washirika, na akataja mifano ya kuwafanya hivyo, nayo imefichikana (hiyo shirki) kuliko athari (kishindo cha kukanyaga) cha sisimizi juu ya jiwe jeusi katika giza nene la usiku, kisha akataja mifano juu ya hilo: nayo ni mtu kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, na kubwa zaidi kuliko hilo ni kumsawazisha huyo na Mwenyezi Mungu ukasema: Namuapa Mwenyezi Mungu na maisha yangu, au ukaitazama sababu bila kumjali msababishaji, na wala usilirudishe jambo kwa Mwenyezi Mungu, ukasema: Lau kama si mbwa huyu anayetulinda basi wangetujia wezi, au mtu akasema: laiti isingekuwa bata hapa nyumbani anayetuzindua anapoingia yeyote mgeni basi wezi wangelitujia, na ni katika shirki pia: kauli ya mtu kumwambia mwenzie: akitaka Mwenyezi Mungu na ukataka, na kauli ya mtu: lau kama si Mwenyezi Mungu na fulani, kisha akatilia mkazo juu ya hayo yote kuwa ni shirki ndogo, na ikiwa ataitakidi kuwa mtu au bata au mbwa ndiyo inayoathiri yenyewe bila Mwenyezi Mungu basi hiyo ni shirki kubwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama