Aina ndogo

Orodha ya Hadithi

Ewe Mola wangu usilifanye kaburi langu kuwa ni sanamu lenye kuabudiwa, zimekuwa kali hasira za Mwenyezi Mungu juu ya watu walioyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mwenye kumuapia asiyekuwa Allah atakuwa amekufuru au kamshirikisha Allah .
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Ninaloliogopea zaidi kwenu nyinyi: ni shirki ndogo, akaulizwa kuhusu hilo, akasema: ni Riyaa (kujionyesha).
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kwani hawaharamishi aliyoyahalalisha Mwenyezi Mungu nanyi mkayaharamisha? na wanahalalisha aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu nanyi mkayahalalisha? Nikasema: Ndivyo, Akasema: Basi huko ndiko kuwaabudu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Yakwamba Mtume rehema na Amani zimfikie aliulizwa kuhusu Nushra (kutibu uchawi kwa uchawi)? Akasema: Hiyo ni katika kazi za shetani.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Itakayemrudisha imani ya mkosi wa ndege akaacha shida yake basi atakuwa amefanya shirki, wakasema: Ni ipi kafara ya hilo? Akasema: ni useme: Ewe Mwenyezi Mungu hakuna kheri ila kheri yako, na hakuna ndege ispokuwa ndege wako, na hakuna Mola zaidi yako.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Atakayekutana na Mwenyezi Mungu hali yakuwa hamshirikishi na chochote ataingia peponi, na atakaye kutananaye hali yakuwa anamshirikisha na chochote ataingia motoni.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Katika kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:- "Na wakasema msiwaache waungu wenu, wala msimuache Wadda, wala Suwa'u wala Yaghuth na Yauq na Nasr" Amesema Ibn Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Haya ni majina ya watu wema katika watu wa Nuhu.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Msimfanyie Mwenyezi Mungu washirika na hali nyinyi mnajua, Amesema bin Abbas katika aya hii: Washirika, ni ushirikina, uliofichikana kuliko sauti ya mkanyago wa mdudu chungu katika jiwe kubwa jeusi katika giza nene la usiku.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa
Mikosi ya ndege ni shirki, na hakuna yeyote miongoni mwetu ispokuwa (ana chembe ya hilo), lakini Mwenyezi Mungu huliondoa kwa kumtegemea
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa