عن ابن عباس رضي الله عنهما في قول الله تعالى : (وَقَالُوا لا تَذَرُنَّ آلِهَتَكُمْ وَلا تَذَرُنَّ وَدًّا وَلا سُوَاعًا وَلا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسْرًا) قال: "هذه أسماء رجال صالحين من قوم نوح، فلما هَلَكوا أَوحى الشَّيطان إلى قَومِهِم أنِ انْصِبُوا إلى مَجَالِسِهِم الَّتي كانوا يَجْلِسون فيها أنصَابًا، وسَمُّوها بأسمَائِهِم، فَفَعَلُوا، ولم تُعْبَد، حتَّى إِذَا هَلَك أُولئك ونُسِيَ العلم عُبِدت".
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ibn Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao-Katika kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:- "Na wakasema msiwaache waungu wenu, wala msimuache Wadd, wala Suwa'u wala Yaghuth na Yauq na Nasr" Akasema: "Haya ni majina ya watu wema katika watu wa Nuhu, walipokufa shetani aliwajulisha watu wao kuwa wekeni katika vikao vyao ambavyo walikuwa wakikaa hapo masanamu, na yaiteni kwa majina yao, wakafanya hivyo, na hayakuabudiwa, mpaka walipokufa hao na elimu ikasahaulika yakaabudiwa".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Ana tafsiri Ibn Abbas radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Aya hii tukufu kuwa miungu hii ambayo ameitaja Mwenyezi Mungu Mtukufu- Kuwa watu wa Nuhu waliusiana kuendelea kuiabudu baada ya kuwa amewakataza Nabii wao Nuhu ziwe juu yake sala na salamu- kutomshirikisha Mwenyezi Mungu- kuwa majina hayo asili yake ni majina ya watu wema miongoni mwao, walichupa mipaka ndani yake kwa ushawishi wa Ibilisi kwao mpaka wakatundika picha zao, Basi jambo likakuwa katika picha hizi mpaka yakawa masanamu yanaabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani Pashto Kiassam Albanian
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa kuchupa mipaka kwa watu wema ni sababu ya kuwabudu kinyume na Mwenyezi Mungu na kuiacha dini moja kwa moja.
  2. Tahadhari ya kupiga picha na kutundika picha, hasa hasa picha za waheshimiwa.
  3. Tahadhari kutokana na vitimbi vya shetani na kuileta kwake batili katika sura ya haki.
  4. Tahadhari kutokana na uzushi na mambo ya kuzua hata kama lengo la mfanyaji litakuwa zuri.
  5. Nikuwa kupiga picha ni katika nyenzo zinazopelekea katika shirki, hivyo ni lazima kutahadhari kupiga picha za viumbe vyenye roho.
  6. Kujua thamani ya uwepo wa elimu na madhara ya kukosekana kwake.
  7. Nikuwa sababu ya kukosekana kwa elimu ni kufa wanachuoni.
  8. Kutahadhari na kuiga, nakuwa hilo linaweza kumpelekea mfanyaji wake katika kutoka katika Uislamu.
  9. Kutangulia shirki katika umma zilizotangulia.
  10. Nikuwa majina haya matano yaliyotajwa ni katika viabudiwa vya watu wa Nuhu.
  11. Kubainishwa kubebana na kusaidiana watu wa batili juu ya batili yao.
  12. Kufaa kuwaombea mabaya makafiri kwa njia ya ujumla.