عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "هلك المُتَنَطِّعون -قالها ثلاثا-".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Masudi-Radhi za Allah ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- " Amesema: Wameangamia wenye kujilazimisha -Alilisema hilo mara tatu-"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anaweka wazi Mtume rehema na Amani zimfikie kuwa kujikita na kujilazimisha katika mambo na kuvuka mpaka ndani yake inakuwa ni sababu ya kuangamia, na makusudio yake rehema na Amani zimfikie ni kulikataza hilo, na miongoni mwa hilo ni kuichosha nafsi katika ibada mpaka ichukie na ivunjike moyo, na miongoni mwa hilo ni kujilazimisha katika mazungumzo na kujikalifisha ndani yake, na katika namna kubwa zaidi za kujilazimisha na ovu zaidi, na inayotakiwa kutahadharishwa zaidi: ni kuchupa mipaka katika kuwatukuza watu wema mpaka katika kiwango ambacho kitapelekea katika ushirikina.