عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "هلك المُتَنَطِّعون -قالها ثلاثا-".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Masudi-Radhi za Allah ziwe juu yake- Yakwamba Mtume -Rehma na amani ziwe juu yake- " Amesema: Wameangamia wenye kujilazimisha -Alilisema hilo mara tatu-"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaweka wazi Mtume rehema na Amani zimfikie kuwa kujikita na kujilazimisha katika mambo na kuvuka mpaka ndani yake inakuwa ni sababu ya kuangamia, na makusudio yake rehema na Amani zimfikie ni kulikataza hilo, na miongoni mwa hilo ni kuichosha nafsi katika ibada mpaka ichukie na ivunjike moyo, na miongoni mwa hilo ni kujilazimisha katika mazungumzo na kujikalifisha ndani yake, na katika namna kubwa zaidi za kujilazimisha na ovu zaidi, na inayotakiwa kutahadharishwa zaidi: ni kuchupa mipaka katika kuwatukuza watu wema mpaka katika kiwango ambacho kitapelekea katika ushirikina.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhimizwa juu ya kuepuka kujilazimisha katika kila kitu; hasa hasa katika ibada na kuwaheshimu watu wema.
  2. Ukubwa wa pupa yake juu ya kuuokoa umma, na jitihada zake katika kufikisha -Rehema na Amani zimfikie-.
  3. Kuharamishwa kujilazimisha katika mambo yote.
  4. Inapendeza kulitilia mkazo jambo lenye umuhimu.
  5. Kuhimizwa juu ya kulingana sawa katika kila kitu.
  6. Upole wa Uislamu na wepesi wake.
Ziada