عن عائشة رضي الله عنها ، قالت: لما نُزِلَ برسول الله صلى الله عليه وسلم ، طَفِقَ يَطْرَحُ خَمِيصَةً له على وجهه، فإذا اغْتَمَّ بها كشفها فقال -وهو كذلك-: "لَعْنَةُ الله على اليهود والنصارى، اتخذوا قبور أنبيائهم مساجد -يُحَذِّرُ ما صنعوا".
ولولا ذلك أُبْرِزَ قَبْرُهُ، غير أنه خَشِيَ أن يُتَّخَذَ مسجدا.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Amesema: alipofikwa na Mauti Mtume rehema na Amani zimfikie, akawa anarusha nguo yake juu ya uso wake, kila ikimfunika anaifunua, na anasema naye akiwa katika hali hiyo- "Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mayahudi na Wakristo, waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa misikiti- Akitahadharisha waliyoyafanya" Na lau kama isingekuwa hivyo basi lingedhihirishwa kaburi lake, Isipokuwa alihofia kufanywa kuwa msikiti.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anatueleza Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuwa yalipomfika mauti Mtume rehema na Amani zimfikie, alisema naye akiwa katika sakaratil mauti (ulevi wa mauti) "Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mayahudi na Wakristo;" na hiyo ni kwasababu wao walijenga juu ya makaburi ya Manabii wao misikiti, kisha akafafanua Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuwa yeye anakusudia kwa kauli hiyo kuutahadharisha umma wake kutokuangukia katika yale waliyoangukia Mayahudi na Wakristo ukajengwa juu ya kaburi lake msikiti, kisha akabainisha kuwa kilichowazuia maswahaba wasimzike nje ya chumba chake ni hofu yao ya kufanywa kaburi lake kuwa msikiti.