عن عائشة رضي الله عنها ، قالت: لما نُزِلَ برسول الله صلى الله عليه وسلم ، طَفِقَ يَطْرَحُ خَمِيصَةً له على وجهه، فإذا اغْتَمَّ بها كشفها فقال -وهو كذلك-: "لَعْنَةُ الله على اليهود والنصارى، اتخذوا قبور أنبيائهم مساجد -يُحَذِّرُ ما صنعوا". ولولا ذلك أُبْرِزَ قَبْرُهُ، غير أنه خَشِيَ أن يُتَّخَذَ مسجدا.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Amesema: alipofikwa na Mauti Mtume rehema na Amani zimfikie, akawa anarusha nguo yake juu ya uso wake, kila ikimfunika anaifunua, na anasema naye akiwa katika hali hiyo- "Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mayahudi na Wakristo, waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa misikiti- Akitahadharisha waliyoyafanya" Na lau kama isingekuwa hivyo basi lingedhihirishwa kaburi lake, Isipokuwa alihofia kufanywa kuwa msikiti.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anatueleza Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuwa yalipomfika mauti Mtume rehema na Amani zimfikie, alisema naye akiwa katika sakaratil mauti (ulevi wa mauti) "Laana za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Mayahudi na Wakristo;" na hiyo ni kwasababu wao walijenga juu ya makaburi ya Manabii wao misikiti, kisha akafafanua Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kuwa yeye anakusudia kwa kauli hiyo kuutahadharisha umma wake kutokuangukia katika yale waliyoangukia Mayahudi na Wakristo ukajengwa juu ya kaburi lake msikiti, kisha akabainisha kuwa kilichowazuia maswahaba wasimzike nje ya chumba chake ni hofu yao ya kufanywa kaburi lake kuwa msikiti.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kukatazwa kuyafanya makaburi ya Manabii na watu wema kuwa Misikiti inayoswaliwa kwaajili ya Mwenyezi Mungu, kwasababu hilo ni njia inayopelekea katika ushirikina.
  2. Kutilia umuhimu sana Mtume rehema na Amani zimfikie na kuizingatia kwake sana tauhidi na hofu yake juu ya kutukuzwa kaburi lake, kwasababu hilo linapelekea katika ushirikina.
  3. Kufaa kuwalaani Mayahudi na Wakristo na yeyote atakayefanya mfano wa kitendo chao katika kuyajengea makaburi na kuyafanya kuwa Misikiti.
  4. Kubainishwa kwa hekima ya kuzikwa Mtume rehema na Amani zimfikie ndani ya nyumba yake, nakuwa hilo ni kwasababu ya kuzuia kufitinika naye.
  5. Alikuwa Mtume rehema na Amani zimfikie ni mwanadamu, yanatokea kwake yanayotokea kwa wanadamu wengine kama kifo na maumivu ya kutolewa roho.
  6. Pupa ya Mtume Rehma na amani za Allah ziwe juu yake Juu ya umma wake:
  7. Kufaa kuwalaani makafiri kwa njia ya ujumla.
  8. Uharamu wa kuyajengea makaburi kwa ujumla.
  9. Hili ni jibu kwa wale wanaoruhusu kuyajengea makaburi ya wanachuoni na kuyatofautisha na ya wengine.
  10. Ilikuwa kujenga juu ya makaburi ni utaratibu wa Mayahudi na Wakristo.
  11. Kubainishwa utambuzi wa Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake.