عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قلت: يارسول الله، "من أسعد الناس بشفاعتك؟ قال: من قال لا إله إلا الله خالصا من قلبه".
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, "Ni nani atakayefurahika zaidi kwa utetezi wako? Akasema: Atakayesema Laa ilaaha illa llaahu (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu) kwa nia safi toka moyoni mwake.
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Alimuuliza Abuu Huraira Mtume rehema na Amani zimfikie kuhusu mtu atakayefurahika zaidi kwa utetezi wake -rehema na Amani zimfikie- na mwenye hatua nyingi zaidi za kuuendea akamueleza- rehema na Amani zimfikie- kuwa ni wale waliosema shahada hii, nayo ni kushuhudia kuwa hapana Mola apasae kuabudiwa kwa hakiispokuwa Mwenyezi Mungu, na Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kwa utakasifu kutoka moyoni, usiochanganyika na shirki wala kujionyesha.