عن جندب بن عبد الله رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : "قال رجل: والله لا يغفر الله لفلان، فقال الله: من ذا الذي يتألى عليَّ أن لا أغفر لفلان؟ إني قد غفرت له، وأحبطت عملك". وفي حديث أبي هريرة: أن القائل رجل عابد، قال أبو هريرة: "تكلم بكلمة أوبقت دنياه وآخرته".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jundabi bin Abdillahi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Alisema mtu mmoja, Wallahi -Namuapa Mwenyezi Mungu- hatomsamehe Mwenyezi Mungu fulani, Akasema Mwenyezi Mungu: Ninani anayejiapiza kwangu kuwa sitomsamehe fulani? Hakika mimi nimemsamehe, na nimeyaporomosha matendo yako". Na katika hadithi ya Abuu Huraira: Nikuwa msemaji hapa alikuwa ni mtu mchamungu, Amesema Abuu Huraira: "Alizungumza neno moja lililoteketeza dunia yake na Akhera yake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa njia ya kutahadharisha juu ya hatari ya ulimi, kuwa mtu mmoja aliapa kuwa Mwenyezi Mungu hatomsamehe mtu mmoja aliyekuwa akitenda madhambi; kana kwamba kamuhukumia Mwenyezi Mungu na kamfungia maamuzi; alipoamini ndani ya nafsi yake kuwa yeye kwa Mwenyezi Mungu ana ubora na thamani na nafasi, na kwa huyu mkosefu ana udhalili, na huku ni kumuelekeza Mwenyezi Mungu na ni utovu wa adabu kwake, akamuwajibishia mtu huyo tabu na hasara Duniani na Akhera.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama