عن جندب بن عبد الله رضي الله عنه قال: سمعت النبي صلى الله عليه وسلم قبل أن يموت بخمس، وهو يقول: «إني أبرأ إلى الله أن يكون لي منكم خليل، فإن الله قد اتخذني خليلا كما اتخذ إبراهيم خليلا، ولو كنت متخذا من أمتي خليلا لاتخذت أبا بكر خليلا، ألا وإن من كان قبلكم كانوا يتخذون قبور أنبيائهم مساجد، ألا فلا تتخذوا القبور مساجد، فإني أنهاكم عن ذلك».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Jundub bin Abdillah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, Amesema: Nilimsikia Mtume rehema na Amani zimfikie kabla hajafa kwa siku tano: naye akisema: "Hakika mimi najiepusha kwa Mwenyezi Mungu kuwa kwangu kati yenu na rafiki wa ndani, kwani Mwenyezi Mungu amenifanya mimi kuwa kipenzi wa ndani kama alivyomfanya Ibrahim kuwa kipenzi wa ndani, na lau kama ningejifanyia kipenzi wa ndani katika umma wangu basi ningemfanya Abuubakari kuwa kipenzi wa ndani, Fahamuni kuwa hakika wale waliyokuwa kabla yenu waliyafanya makaburi ya Manabii wao kuwa Misikiti, Tambueni kuwa, msiyafanye makaburi kuwa Misikiti, kwani hakika mimi ninakukatazeni na hilo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anazungumza rehema na Amani ziwe juu yake kabla ya kifo chake, kwa umma wake kwa mazungumzo muhimu, akaeleza nafasi yake mbele ya Mwenyezi Mungu nakuwa imefikia daraja nyingi za mapenzi kama alivyoipata Ibrahim Amani iwe juu yake, na kwaajili hiyo akakanusha kuwa na kipenzi mwingine wa ndani zaidi ya Mwenyezi Mungu; kwasababu moyo wake umejaa mapenzi yake na kumtukuza kwake na kumjua kwake, hivyo haufunguki kwa yeyote, na mapenzi ya ndani katika moyo wa kiumbe hayawi ila kwa mmoja, na lau kama angekuwa na kipenzi wa ndani katika viumbe basi angekuwa Abuubakari Swiddiq radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, nayo ni ishara juu ya ubora wa Abuubakari na kumfanya kuwa kiongozi baada yake, kisha akaeleza kuchupa mipaka kwa Mayahudi na Wakristo katika makaburi ya Manabii wao mpaka wakayageuza kuwa viabudiwa vya kishirikina, na akaukataza umma wake wasifanye mfano wa vitendo vyao, na wakristo hawana ispokuwa Nabii mmoja naye ni Isa (Yesu), lakini wanaamini kuwa anakaburi ardhini, na usahihi nikuwa Isa Amani iwe juu yake alinyanyuliwa na wala hakusulubiwa na wala hakuzikwa.