عن علي بن الحسين: "أنه رأى رجلا يجيء إلى فُرْجَةٍ كانت عند قبر النبي صلى الله عليه وسلم فيدخل فيها فيدعو، فنهاه، وقال: ألا أحدثكم حديثا سمعته من أبي عن جدي عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال:« لا تتخذوا قبري عيدا، ولا بيوتكم قبورا، وصلوا علي، فإن تسليمكم يبلغني أين كنتم».
[صحيح بطرقه وشواهده] - [رواه ابن أبي شيبة]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ally bin Husein: "Yakwamba yeye aliona mtu mmoja anakuja toka katika kiupenyo kidogo kilikuwa katika kaburi la Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- anaingia na anaomba hapo, akamkataza, na akasema: Hivi nikusimulieni hadithi niliyoisikia toka kwa baba yangu toka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- amesema: "Msilifanye kaburi langu kuwa sikukuu, wala nyumba zenu kuwa makaburi, na nitakieni rehma, kwani dua zenu hunifikia popote mlipo".
Ni sahihi kwa njia zake na ushahidi wake - Imepokelewa na Ibn Abii Shaybah

Ufafanuzi

Anatueleza Ally bin Husein -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba yeye alimuona mtu mmoja akimuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kaburi la Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, nakuwa yeye alimkataza juu ya hilo kwa ushahidi wa hadithi ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ambayo limekuja ndani yake katazo la kulifanyia mazoea kaburi lake kwa ziara, na katazo la kuzitelekeza nyumba kwa kutokuwa na ibada ya Mwenyezi Mungu ndani yake na dhikri, na kuifananisha kwake na kaburi, na akaeleza kuwa salamu ya muislamu itamfikia yeye -Rehema na Amani ziwe juu yake- mahala popote atakapokuwa muislamu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama