عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما عن رسول الله -صلى الله عليه وآله وسلم- فيما يرويه عن ربه -تبارك وتعالى- قال: «إن الله كَتَبَ الحسناتِ والسيئاتِ ثم بَيَّنَ ذلك، فمَن هَمَّ بحسنةٍ فَلم يعمَلها كَتبها الله عنده حسنةً كاملةً، وإن هَمَّ بها فعمِلها كتبها اللهُ عندَه عشرَ حسناتٍ إلى سَبعِمائةِ ضِعْفٍ إلى أضعافٍ كثيرةٍ، وإن هَمَّ بسيئةٍ فلم يعملها كتبها الله عنده حسنة كاملة، وإن هَمَّ بها فعمِلها كتبها اللهُ سيئةً واحدةً».
زاد مسلم: «ولا يَهْلِكُ على اللهِ إلا هَالِكٌ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao kutoka kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake yeye na familia yake- Katika yale anayoyapokea kutoka kwa Mola wake- Aliyetakasika na kutukuka- Amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika mema na mabaya kisha akalibainisha hilo, atakayepania kufanya jema kisha akawa hakulifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake jema kamili, na akilipania na akalifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake kuwa ni mema kumi mpaka kufikia ziada ya mia saba mpaka ziada nyingi zaidi, na ikiwa atapania kufanya baya na akawa hakulifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake kuwa ni jema kamili, na akilipania na akalifanya analiandika Mwenyezi Mungu kuwa ni baya moja" akaongeza Muslim: "Na haangamii kwa Mwenyezi Mungu ispokuwa mwenye kuangamia".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Katika hadithi hii tukufu nikuwa kupania kufanya jema pamoja na kupupia kulifanya huandikwa jema hata kama halijafanyika, na likifanyika jema moja basi huzidishwa mpaka mara kumi mfano wake mpaka ziada nyingi zaidi, na atakayepania kufanya baya kisha akaliacha kwaajili ya Mwenyezi Mungu huandikwa kwake kuwa ni jema, na atakayefanya baya moja basi litaandikwa baya moja, na atakayepania kufanya baya kisha akaliacha hakuandikwi chochote, na yote hayo yanaonyesha upana wa rehma za Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, kiasi kwamba amewafadhilisha kwa fadhila hizi na kwa kheri nyingi.