عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما عن رسول الله -صلى الله عليه وآله وسلم- فيما يرويه عن ربه -تبارك وتعالى- قال: «إن الله كَتَبَ الحسناتِ والسيئاتِ ثم بَيَّنَ ذلك، فمَن هَمَّ بحسنةٍ فَلم يعمَلها كَتبها الله عنده حسنةً كاملةً، وإن هَمَّ بها فعمِلها كتبها اللهُ عندَه عشرَ حسناتٍ إلى سَبعِمائةِ ضِعْفٍ إلى أضعافٍ كثيرةٍ، وإن هَمَّ بسيئةٍ فلم يعملها كتبها الله عنده حسنة كاملة، وإن هَمَّ بها فعمِلها كتبها اللهُ سيئةً واحدةً». زاد مسلم: «ولا يَهْلِكُ على اللهِ إلا هَالِكٌ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillahi bin Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao kutoka kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake yeye na familia yake- Katika yale anayoyapokea kutoka kwa Mola wake- Aliyetakasika na kutukuka- Amesema: "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika mema na mabaya kisha akalibainisha hilo, atakayepania kufanya jema kisha akawa hakulifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake jema kamili, na akilipania na akalifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake kuwa ni mema kumi mpaka kufikia ziada ya mia saba mpaka ziada nyingi zaidi, na ikiwa atapania kufanya baya na akawa hakulifanya analiandika Mwenyezi Mungu kwake kuwa ni jema kamili, na akilipania na akalifanya analiandika Mwenyezi Mungu kuwa ni baya moja" akaongeza Muslim: "Na haangamii kwa Mwenyezi Mungu ispokuwa mwenye kuangamia".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi hii tukufu nikuwa kupania kufanya jema pamoja na kupupia kulifanya huandikwa jema hata kama halijafanyika, na likifanyika jema moja basi huzidishwa mpaka mara kumi mfano wake mpaka ziada nyingi zaidi, na atakayepania kufanya baya kisha akaliacha kwaajili ya Mwenyezi Mungu huandikwa kwake kuwa ni jema, na atakayefanya baya moja basi litaandikwa baya moja, na atakayepania kufanya baya kisha akaliacha hakuandikwi chochote, na yote hayo yanaonyesha upana wa rehma za Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka, kiasi kwamba amewafadhilisha kwa fadhila hizi na kwa kheri nyingi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kubainishwa fadhila za Mwenyezi Mungu mtukufu juu ya umma huu, kwani laiti yasingelikuwa yaliyotajwa katika hadithi basi mtihani ungekuwa mkubwa, kwasababu matendo ya waja katika maovu ni mengi.
  2. Malaika waangalizi wanaandika matendo ya moyoni, tofauti na wale waliosema kuwa wao hawaandiki ispokuwa matendo ya wazi.
  3. Kuthibitisha kuandikwa kwa mema na mabaya kwa kutokea kwake na thawabu na adhabu, kwa kauli yake: "Hakika Mwenyezi Mungu ameandika mema na mabaya".
  4. Mema yanayotokea na mabaya yanayotokea tayari yamekwisha malizwa na yameandikwa na yametulia, na waja wanafanya kwa matashi yao kulingana na yale yaliyoandikwa kwao.
  5. Kuthibitisha matendo ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kauli yake: "Ameandika" Ni sawa sawa tukisema kuwa yeye aliamrisha yaandikwe, au ameandika yeye mwenyewe Mtukufu, kwa kuja hadithi zingine katika hilo, mfano kauli yake rehema na Amani ziwe juu yake: "Na akaiandika Taurati kwa mkono wake" bila kufananisha wala kuleta tafsiri.
  6. Kuwajali Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka viumbe, kiasi kwamba aliandika mema yao na mabaya yao katika makadirio na katika sheria.
  7. Kuzingatiwa nia katika matendo na athari yake.
  8. Kufafanua baada ya kuzungumza kwa ujumla ni katika ufasaha.
  9. Kupania kufanya jema huandikwa jema kamili.
  10. Fadhila za Mwenyezi Mungu Mtukufu na upole wake na wema wake, kuwa mwenye kupania kufanya jema na akawa hakulifanya analiandika Mwenyezi Mungu kuwa ni jema, Na atakayepania kufanya baya akaliacha kwaajili ya Mwenyezi Mungu linaadikwa kwake kuwa ni jema, na makusudio ya kupania: Ni kuazimia, si tu ilimradi minong'ono ya nafsi.