عن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما يبلغ به النبي صلى الله عليه وسلم : «الرَّاحمون يرحَمُهمُ الرحمنُ، ارحموا أهلَ الأرضِ، يرحمْكم مَن في السماءِ».
[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Amri- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Anamfikishia Mtume rehema na Amani ziwe juu yake-: "Wenye huruma huwahurumia Ar-Rahmani -Mwingi wa huruma-, wahurumieni watu wa ardhini atakuhurumieni aliyeko mbinguni".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy
"Wenye huruma" Ambao wanawahurumia walioko ardhini miongoni mwa wanadamu na wanyama wenye kuwaheshimu na kuwahurumia na kuwafanya wema na kuwafariji "Huwahurumia mwingi wa huruma" neno hili limetokana na huruma nayo inajulikana, na miongoni mwa hilo ni awafanyie wema na awapendelee, na malipo huendana na matendo. "Wahurumieni walioko ardhini" Ameleta neno la kiujumla ili liwahusu viumbe wote, ili amuhurumie mwema na muovu na wanyama na ndege, "Atakuhurumieni aliyeko mbinguni" Yaani: Atakuhurumieni Mwenyezi Mungu Mtukufu aliyeko mbinguni, na hairuhusiwi kuleta tafsiri tofauti kwa kusema kuwa makusudio ya aliyeko mbinguni maana yake ni ufalme wake na mengineyo; kwasababu kuwa juu ya viumbe vyake Mwenyezi Mungu kumethibiti kwa Qur'ani na mafundisho ya Mtume na makubaliano ya umma, na hatumaanishi katika kauli yetu kuwa "Mwenyezi Mungu yuko mbinguni" kuwa mbingu zinamzunguka na yeye yuko ndani yake, Ametukuka Mwenyezi Mungu na hilo, Bali neno Fii "katika" linamaana ya "juu" yaani: juu ya mbingu juu zaidi ya viumbe vyake vyote.