+ -

عن عبد الله بن عمرو رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال:
«الرَّاحِمُونَ يَرْحَمُهمُ الرَّحمنُ، ارحَمُوا أهلَ الأرضِ يَرْحْمْكُم مَن في السّماء».

[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وأحمد] - [سنن أبي داود: 4941]
المزيــد ...

Imepokewa Kutoka kwa Abdallah Ibn Amri -Radhi za Allah ziwe juu yao wawili- yakwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Wenye huruma huwahurumia Ar-Rahmani -Mwingi wa huruma-, wahurumieni walioko ardhini atakuhurumieni aliyeko mbinguni."

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa wale wenye kuwahurumia wenzao huwahurumia Rahman -Mwingi wa rehema- kwa huruma yake iliyokienea kila kitu; Yakiwa ni malipo sawa na matendo yao.
Kisha akaamrisha -Rehema na amani ziwe juu yake-kuwahurumia wote walioko ardhini kwanzia binadamu au wanyama au ndege, au wengineo katika aina ya viumbe mbali mbali, na malipo ya hilo; mtahurumiwa na Mwenyezi Mungu kutoka juu ya mbingu yake ya saba.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية القيرقيزية النيبالية اليوروبا الليتوانية الدرية الصومالية الكينياروندا التشيكية المالاجاشية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Dini ya Uislamu ni dini ya huruma, na dini nzima imesimama katika kumtii Mwenyezi Mungu na kuwatendea wema viumbe.
  2. Mwenyezi Mungu aliyetakasika na kutukuka anasifika kwa sifa ya huruma, naye Mtukufu ni Mwingi wa rehema mwenye kurehemu, mfikishaji wa huruma kwa waja wake.
  3. Malipo huendana na matendo, wenye huruma huwahurumia Rahman -Mwingi wa rehema-.