عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «كان رجل يُدَايِنُ الناس، وكان يقول لفَتَاه: إذا أَتَيْتَ مُعْسِرًا فَتَجَاوَزْ عنه، لعَلَّ الله أن يَتَجَاوَزَ عنَّا، فَلَقِيَ الله فتَجَاوز عنه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Alikuwa mtu mmoja akiwadai watu, na alikuwa akimwambia kijana wake: Ukimuendea mwenye hali ngumu msamehe, huenda Mwenyezi Mungu akatusamehe na sisi, akakutana na Mwenyezi Mungu akamsamehe".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Maana ya hadithi: "Alikuwa mtu mmoja akiwadai watu" Yaani: Akifanya miamala ya mkopo. au anauza kwa mkopo, na alikuwa akimwambia kijana wake anayekusanya madeni yaliyoko kwa watu: Ukifika kwa mdaiwa na akawa hana cha kulipa deni analodaiwa kwa kushindwa kwake. "Msamehe" Ima kwa kumpa muda na kutong'ang'ania katika kumdai, au kwa kukubali alichonacho hata kama kina mapungufu kidogo. "Huenda Mwenyezi Mungu akatusamehe" Yaani akatusamehe kwasababu ya kuwasamehe waja waje na kuwarahisishia na kuondoa uzito juu yao. Na hii huenda; ni kwasababu Mwenyezi Mungu huwalipa waja kwa wema wao kwa waja wake kwa yale yanayoendana na matendo yao. Na huenda ni kwa kujua kwake kuwa Mwenyezi Mungu hapotezi matendo ya yeyote atakayefanya matendo mazuri. "Akakutana na Mwenyezi Mungu akamsamehe" ni malipo yake kwa huruma yake kwa watu, na upole wake kwao, na kuwarahisishia kwake wao, pamoja nakuwa yeye hajafanya amali yoyote kabisa kama ilivyokuja katika riwaya ya Nasai na Ibni Hibban: "Hakika kuna mwanaume hakufanya amali yoyote kabisa, na alikuwa akiwadai watu, anamwambia mjumbe wake: Chukua kinachowezekana, na acha kinachoshindikana na samehe, huenda Mwenyezi Mungu akatusamehe na sisi".Alipomdhania vizuri Mwenyezi Mungu Mtukufu- Na akawafanyia wema waja wa Mwenyezi Mungu Mtukufu- Mwenyezi Mungu akamsamehe makosa yake, na malipo huendana na matendo.