Orodha ya Hadithi

Hakika katika watu waovu zaidi ni wale watakaokutwa na Kiyama wakiwa hai, na mwenye kuyafanya makaburi kuwa mahala pa kusalia
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
, atamuingiza Mwenyezi Mungu peponi kulingana na yale aliyokuwa nayo katika matendo
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atakayempa muda mwenye hali ngumu, au akamfutia deni, Allah atampa kivuli siku ya kiyama chini ya kivuli cha Arshi yake siku ambayo hapatokuwa na kivuli isipokuwa kivuli chake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika nyinyi mtamuona Mola wenu kama mnavyouona mwezi huu, hamtokingwa katika kumuona kwake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika imefikia wakati ambao mtu atafikiwa na hadithi yangu akiwa amekaa kwenye tandiko lake na akisema: Hakika kitakachotuhukumu kati yetu ni kitabu cha Mwenyezi Mungu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika Mwenyezi Mungu atamchagua mtu mmoja katika umma wangu mbele ya mkusanyiko wa watu siku ya Kiyama
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mwenyezi Mungu alipoumba Pepo na Moto alimtuma Malaika Jibril -Amani iwe juu yake- aende peponi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
La kwanza litakalohukumiwa kati ya watu siku ya kiyama ni katika damu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika hao wawili wanaadhibiwa, na hawaadhibiwi kwa makosa makubwa, ama mmoja wao alikuwa hajistiri na mkojo, na ama mwingine alikuwa akitembea kwa kuchonganisha watu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Wewe pamoja na uliyempenda
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi nikuhadithieni hadithi kuhusu Dajali ambayo hajawahi kuhadithia Nabii yeyote watu wake! Hakika yeye ni chongo, na hakika yeye atakuja akiwa pamoja na mfano wa pepo na moto, anayoisema kuwa ni pepo huo ndio moto
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu, Ole wao waarabu kutokana na shari iliyokaribia, imefunguliwa leo katika ngome ya Ya-ajuju na Ma-juju mfano wa hiki, na akachora duara kwa vidole vyake viwili, kidole gumba na kile kinachofuata, nikasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hivi tunaweza kuangamizwa hali miongoni mwetu kuna wema? Akasema: Ndiyo, pindi uchafu utakapokithiri.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Nyanyua kichwa chako na sema yasikilizwe, na omba upewe, na taka utetezi utetewe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi nisikuelezeni watu wa peponi? Kila mnyonge mwenye kujishusha, na lau kama angeliapia kwa Mwenyezi Mungu basi angelimuepusha na kila linalompa uzito, Hivi nisikuelezeni watu wa motoni? kila jeuri mkali mwenye kiburi.
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika peponi kuna daraja mia moja kaziandaa Mwenyezi Mungu kwaajili ya wenye kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu kati ya daraja mbili ni kama masafa ya baina ya mbingu na ardhi
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakika atakuja mtu mnene tena mkubwa siku ya kiyama akiwa halingani mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hiyo ndiyo kauli yake Mtukufu: "Huwapa umakinifu Mwenyezi Mungu wale walioamani kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Atasogezwa muumini siku ya kiyama kwa Mola wake mpaka aweke upande wake kwake, kisha amtake akiri makosa yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hautonyanyuka unyayo wa mja siku ya Kiyama mpaka aulizwe kuhusu umri wake aliumaliza katika mambo yapi? Na kuhusu elimu yake aliifanyia kazi katika nini? Na kuhusu mali yake ni wapi aliichuma? Na aliitoa katika mambo gani? Na kuhusu mwili wake aliumaliza katika mambo yapi?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Litafikia jambo hili ulipofika usiku na mchana, na wala hatoacha Mwenyezi Mungu nyumba ya mjini wala ya kijijini isipokuwa ataiingiza Mwenyezi Mungu dini hii
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika Mwenyezi Mungu hamdhulumu muumini kwa jema alilofanya, huandikiwa thawabu za wema wake hapa Duniani na hulipwa thawabu hizo huko Akhera
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika miongoni mwa alama za Kiyama ni kuondolewa elimu, na kuzidi ujinga, na kukithiri uzinifu, unywaji pombe, na wanaume watakuwa wachache na wanawake watakuwa wengi mpaka itafikia wanawake hamsini kusimamiwa na mwanaume mmoja
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitosimama Kiyama mpaka apite mtu juu ya kaburi la mtu aseme: Natamani ningekua nafasi yake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitasimama Kiyama mpaka mpigane na Mayahudi, mpaka jiwe ambalo nyuma yake kuna Myahudi liseme: Ewe Muislamu huyu hapa Myahudi nyuma yangu njoo umuuwe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hivi karibuni atakuteremkieni Issa mwana wa Mariam atakuwa hakimu na muadilifu, atavunja misalaba, na ataua nguruwe, na ataweka kodi (Jizia), na mali itabugujika (itakuwa nyingi) mpaka itafikia mahali hakuna yeyote atakayeikubali
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakita simama Kiyama mpaka jua lichomoze kutoka upande wa Magharibi, na likichomoza na wakaliona watu wote wataamini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hakitosimama kiyama mpaka zama zikaribiane
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ataikamata Mwenyezi Mungu ardhi, na ataikunja mbingu kwa mkono wake wa kulia kisha atasema: Mimi ndiye Mfalme; wako wapi wafalme wa ardhi?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Birika langu ukubwa wake ni sawa na mwendo wa mwezi mzima, maji yake ni meupe kuliko maziwa, na harufu yake ni nzuri kuliko ya Miski
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kwa hakika mimi nitakuwa kwenye Birika langu namtazama kila mwenye kuja kwangu kunywa, na kuna watu watafukuzwa, na nitasema: Ewe Mola wangu huyu anatokana na mimi na ni katika umma wangu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Namuapa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake, kwa hakika vyombo vyake ni vingi kama wingi wa nyota mbinguni na sayari zake
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mauti yataletwa yakiwa kama dume la Kondoo mwenye rangi mchanganyiko ya weusi na weupe
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Moto wenu wa Dunia ni sawa na sehemu tu ya sabini itokanayo na moto wa Jahannam
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Ametuhadithia Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- naye ni mkweli mwenye kukubaliwa: "Kwa hakika mmoja wenu hukusanywa umbile lake kwenye tumbo la mama yake mchana arobaini na nyusiku arobaini
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alitaja jambo fulani, akasema: "Jambo lenye kuogopesha litakuwa wakati itakapo ondoka elimu
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Akasema: "Watahesabiwa kwa hiyana waliyokufanyia na kukuasi na kukudanganya, na itahesabiwa adhabu yako uliyowapa
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Hivi yule aliyemfanya atembee kwa miguu miwili hawezi kumfanya atembee kwa uso wake siku ya Kiyama?
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kisha hakika bila shaka mtakuja kuulizwa kuhusu neema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Kutakuwa mwisho wa umma wangu na watu, wakikuhadithieni mambo ambayo humkuwahi kuyasikia nyinyi wala baba zenu, ole wenu na ole wao
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu
Mtakapo msikia muadhini basi semeni mfano wa yale anayo yasema, kisha mnitakie rehema
عربي Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu