عَنْ أَبِي ذَرٍّ رضي الله عنه قَالَ:
قُلْتُ: يَا رَسُولَ اللهِ مَا آنِيَةُ الْحَوْضِ؟ قَالَ: «وَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَآنِيَتُهُ أَكْثَرُ مِنْ عَدَدِ نُجُومِ السَّمَاءِ وَكَوَاكِبِهَا، أَلَا فِي اللَّيْلَةِ الْمُظْلِمَةِ الْمُصْحِيَةِ، آنِيَةُ الْجَنَّةِ مَنْ شَرِبَ مِنْهَا لَمْ يَظْمَأْ آخِرَ مَا عَلَيْهِ، يَشْخَبُ فِيهِ مِيزَابَانِ مِنَ الْجَنَّةِ، مَنْ شَرِبَ مِنْهُ لَمْ يَظْمَأْ، عَرْضُهُ مِثْلُ طُولِهِ، مَا بَيْنَ عَمَّانَ إِلَى أَيْلَةَ، مَاؤُهُ أَشَدُّ بَيَاضًا مِنَ اللَّبَنِ، وَأَحْلَى مِنَ الْعَسَلِ».

[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abii Dharri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
Nilisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hicho chombo cha Birika kiko vipi? Akasema: "Namuapa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake, kwa hakika vyombo vyake ni vingi kama wingi wa nyota mbinguni na sayari zake eleweni vyema kuwa kung'aa kwake kutakuwa katika usiku usio na mwezi, pako safi, vyombo vya peponi atakaye kunywa katika vyombo hivyo hatopatwa na kiu milele wala kiu hakitomrudia, na maji hayo yanaruka na kububujika kupitia mabomba mawili yaliyo juu ya peponi, yeyote atakaye kunywa katika Birika hilo hatopatwa na kiu, upana wake ni sawa na urefu wake ambao ni sawa kutoka Amman mpaka Aila (Ni katika miji ya Jordan, baina yake ni km 330) maji yake ni meupe mno kuliko maziwa, na ni matamu kuliko asali."

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Ame apa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ya kuwa vyombo vya Birika lake siku ya kiyama, ni vingi kuliko nyota angani, na kuliko sayari za mbinguni, Na hilo litadhihiri katika usiku wenye kiza ambao hauna mwezi, kwa sababu usiku wenye kuangaza huwa hakuna ndani yake nyota zenye kuonekana kwa kujificha kwake kutokana na mwanga wa mwezi, ambao hauna mawingu, kwa sababu kuwepo kwa mawingu kunazuia kuonekana kwa nyota, Na kwa hakika vyombo vya peponi atakaye kunywa miongoni mwa vinywaji vilivyomo humo, inakuwa ndiyo mwisho kabisa kwa mnywaji kupata kinywaji kwa sababu ya kiu, Na Birika lake linachuruzisha kupitia mabomba mawili yatokayo peponi, na upana wake ni sawa na urefu wake; Hivyo Birika nguzo zake zote zipo sawa, urefu wake ni sawa na umbali ambao upo kati ya Amman mji ambao upo Sham mpaka Aila nao ni mji maarufu uliopo pembeni mwa mji wa Sham, Na maji ya Birika ni meupe sana kuliko maziwa, na ladha yake ni tamu zaidi kuliko Asali.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuthibitisha uwepo wa Birika na neema mbalimbali ziliopo humo.
  2. Ukubwa wa Birika na urefu wake na upana wake na wingi wa vyombo vyake.