+ -

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ رضي الله عنهما أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«مَنْ قَالَ حِينَ يَسْمَعُ النِّدَاءَ: اللَّهُمَّ رَبَّ هَذِهِ الدَّعْوَةِ التَّامَّةِ، وَالصَّلاَةِ القَائِمَةِ، آتِ مُحَمَّدًا الوَسِيلَةَ وَالفَضِيلَةَ، وَابْعَثْهُ مَقَامًا مَحْمُودًا الَّذِي وَعَدْتَهُ، حَلَّتْ لَهُ شَفَاعَتِي يَوْمَ القِيَامَةِ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 614]
المزيــد ...

Na kutoka kwa Jaabir bin Abdillah -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake-:
"Atakayesema wakati anasikia adhana: Allaahumma rabba haadhihid da'watit taamma, was swalaatul qaaima, aati Muhammadanil wasiilata wal fadhwiila, wab'ath-huu maqaaman mahmuudanil ladhii wa a'ttah, (Ewe Mwenyezi Mungu, Mola wa wito huu uliotimia, na swala iliyosimama, mpe Muhammad utetezi na fadhila, na umfufue mahali pakusifiwa ulipomuahidi) basi utakuwa halali kwake utetezi wangu siku ya Kiyama".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 614]

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayesema wakati amemsikia muadhini baada ya kumaliza adhana:
"Ewe Mwenyezi Mungu Mola wa wito huu" nayo ni matamshi ambayo hutumika kuita katika ibada ya Mwenyezi Mungu na swala, "Uliotimia" uliokamilika, wito wa tauhidi na ujumbe, "na swala iliyosimama" yenye kudumu ambayo itasimamishwa hivi punde, "mpe" mgawie, "Muhammadi utetezi" na cheo cha juu peponi ambacho hakimstahiki mwingine ila yeye rehema na amani ziwe juu yake, "na fadhila" cheo cha juu zaidi ya vyeo vya viumbe, "na umfufue" na umpe "nafasi yenye kusifiwa" anayosifiwa mwenye kuwanayo; nao ni utetezi mkuu wa siku ya Kiyama, "uliyomuahidi" kwa kauli yako "Huenda akakufufua Mola wako katika nafasi yenye kusifiwa" ili iwe yake Mtume rehema na amani ziwe juu yake.
Atakayeomba dua hii atastahiki kuupata utetezi wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake siku ya Kiyama.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya kuomba dua hii baada ya kumaliza kurudia nyuma ya muadhini, na ambaye hatosikia adhana; basi hatakiwi kuisema.
  2. Ubora wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kiasi kwamba amepewa uwakala na fadhila na nafasi na utetezi mkuu wa kutetea kuhukumiwa baina ya viumbe.
  3. Kuthibitisha utetezi wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake; kwa kauli yake: "Ataupata utetezi wangu siku ya Kiyama".
  4. Utetezi wake rehema na amani ziwe juu yake utakuwa kwa wale waliotenda madhambi makubwa katika umma wake ili wasiingie motoni, au aliyeingia atoke, au katika kuingia peponi pasina hesabu, au kunyanyuliwa daraja aliyeingia.
  5. Amesema Attwayyibi: kuanzia mwanzo wa "Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu" huu ndio wito uliotimia, na maneno "Hayya a'la" (njooni katika) ndio swala iliyosimama katika kauli yake wanasimamisha swala, na inawezekana kuwa makusudio ya swala hapa ni dua, na kwa mujibu wa hili kauli yake "na swala iliyosimama" ni kubainishwa wito uliyotimia, na inawezekana kuwa makusudio yake ni swala iliyozoeleka wanayoitwa kwayo kwa wakati huo, na ndilo lililokaribu na maana halisi.
  6. Amesema Al-Mulhab: Katika hadithi hii kuna himizo la kuomba dua katika nyakati za swala; kwa sababu ni hali zinazotarajiwa zaidi kujibiwa dua.