عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «مَنْ أَنْظَرَ مُعْسِرا، أو وضع له، أظَلَّهُ الله يوم القيامة تحت ظِل عرشه يوم لا ظِلَّ إلا ظِلُّه».
[صحيح] - [رواه الترمذي والدارمي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake: "Atakayempa muda mwenye hali ngumu, au akamsamehe, atampa kivuli Mwenyezi Mungu siku ya kiyama chini ya kivuli cha Arshi yake siku ambayo hakutokuwa na kivuli ispokuwa kivuli chake".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Ameeleza Abuu Huraira kuwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake Amesema: "Atakayempa muda mwenye hali ngumu" Yaani akampa nafasi mdaiwa masikini, kutoa muda ni kuchelewesha kunakotazamiwa kusamehe. Kauli yake "Au akamsamehe" Yaani akamfutia katika deni lake, na katika riwaya ya Abuu Nuaim "Au akampa zawadi". Hivyo malipo ni: "Atampa kivuli Mwenyezi Mungu siku ya kiyama chini ya kivuli cha Arshi yake" Yaani atampa kivuli katika kivuli cha Arshi yake halisia au atamuingiza peponi; Atamkinga Mwenyezi Mungu na joto la siku ya kiyama. Na malipo haya yatakuwa: "Siku ambayo kutokuwa na kivuli ispokuwa kivuli chake" Yaani kivuli cha Mwenyezi Mungu, na hakika amestahiki mtoa muda jambo hilo kwasababu ya kumpendelea mdaiwa kuliko nafsi yake na akampumzisha na Mwenyezi Mungu akampumzisha, na malipo huendana na matendo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kupendeza kukopesha kuzuri na kuamiliana na mdaiwa kwa upole na ulaini.
  2. Kumpa muda mwenye hali ngumu au kumsamehe deni lake lote ni katika mambo yanayopelekea kuwekwa chini ya kivuli cha Ar Rahman- Mwingi wa rehma- siku ambayo hakutokuwa na kivuli ispokuwa kivuli chake.
  3. Ubora wa mwenye kudai mwenye kusamehe na yale anayoyapata katika malipo makubwa Akhera.
  4. Ubora wa kuwafanyia wepesi waja wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  5. Kufaa kufanya miamala ya madeni.
  6. Kufaa kujitolea wakili itakapokuwa ni kwa idhini ya yule anayemuwakilisha.