عَنْ ‌الزُّبَيْرِ بْنِ الْعَوَّامِ قَالَ:
لَمَّا نَزَلَتْ: {ثُمَّ لَتُسْأَلُنَّ يَوْمَئِذٍ عَنِ النَّعِيمِ} [التكاثر: 8]، قَالَ الزُّبَيْرُ: يَا رَسُولَ اللهِ، وَأَيُّ النَّعِيمِ نُسْأَلُ عَنْهُ، وَإِنَّمَا هُمَا الْأَسْوَدَانِ التَّمْرُ وَالْمَاءُ؟ قَالَ: «أَمَا إِنَّهُ سَيَكُونُ».

[حسن] - [رواه الترمذي وابن ماجه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Zubairi bin Awwam amesema:
Ilipoteremka: "Kisha hakika bila shaka mtakuja kuulizwa kuhusu neema" [Takathur: 8], akasema Zubairi: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni neema zipi tutakazooulizwa juu yake, au ni hivi vyeusi viwili tende na maji (Vyakula na vinywaji kwa ujumla)? Akasema: "Hakika bila shaka zitakuwa hizo".

Ni nzuri - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Ilipoteremka aya: "Kisha hakika bila shaka mtaulizwa siku hiyo kuhusu neema" Yaani: Mtakuja kuulizwa kuhusu kutekeleza shukurani kwa yale aliyowaneemesha Mwenyezi Mungu juu yenu miongoni mwa neema, akasema Zubairi bin Awwam radhi za Allah ziwe juu yake: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ni neema zipi tutakazoulizwa juu yake?! Ni neema mbili ambazo hazihitaji kuziomba ambazo ni tende na maji!.
Akasema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: Ama hakika nyinyi mtaulizwa kuhusu neema pamoja hali hii iliyo nayo, ni hizi neema mbili kubwa katika neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Msisitizo wa kumshukuru Mwenyezi Mungu juu ya neema.
  2. Neema ni miongoni mwa vile ambavyo mja ataulizwa kwavyo siku ya Kiyama.