عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«إِنَّ اللهَ لَا يَظْلِمُ مُؤْمِنًا حَسَنَةً، يُعْطَى بِهَا فِي الدُّنْيَا وَيُجْزَى بِهَا فِي الْآخِرَةِ، وَأَمَّا الْكَافِرُ فَيُطْعَمُ بِحَسَنَاتِ مَا عَمِلَ بِهَا لِلَّهِ فِي الدُّنْيَا، حَتَّى إِذَا أَفْضَى إِلَى الْآخِرَةِ، لَمْ تَكُنْ لَهُ حَسَنَةٌ يُجْزَى بِهَا».

[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani ziwe juu yake:
"Kwa hakika Mwenyezi Mungu hamdhulumu muumini kwa jema alilofanya, huandikiwa thawabu za wema wake hapa Duniani na hulipwa thawabu hizo huko Akhera Ama kafiri hulishwa kwa mema aliyoyafanya kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hapa duniani, mpaka akifika Akhera anakuwa hana jema lolote ambalo atalipwa nalo."

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anaweka wazi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- ukubwa wa fadhila za Mwenyezi Mungu kwa waumini, na uadilifu wake kwa makafiri. Ama muumini hazipungui thawabu za mema aliyoyafanya; Bali hulipwa hapa duniani wema kwa utiifu wake, pamoja na kulimbikiziwa malipo yake huko Akhera; Na huenda akahifadhiwa malipo yake yote huko Akhera. Ama kafiri, Mwenyezi Mungu humlipa malipo kutokana na wema alioufanya kwa malipo ya mambo yaliyo mazuri hapa Duniani, mpaka inakuwa akifika Akhera, anakuwa hana thawabu na malipo atakayo lipwa huko, kwa sababu matendo mema ambayo yatamfaa hapa Duniani na Akhera lazima awe mtendaji wake ni muumini.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa yeyote atakaye kufa hali ya kuwa ni kafiri basi matendo yake hayatomfaa.
Ziada