عَنْ حَكِيمِ بْنِ حِزَامٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ، قَالَ:
قُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، أَرَأَيْتَ أَشْيَاءَ كُنْتُ أَتَحَنَّثُ بِهَا فِي الجَاهِلِيَّةِ مِنْ صَدَقَةٍ أَوْ عَتَاقَةٍ، وَصِلَةِ رَحِمٍ، فَهَلْ فِيهَا مِنْ أَجْرٍ؟ فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «أَسْلَمْتَ عَلَى مَا سَلَفَ مِنْ خَيْرٍ».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Hakiim Bin Hizaam -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema:
Nilisema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni upi mtazamo wako katika mambo ambayo nilikuwa nikifanya ibada kupitia mambo hayo kabla ya kuwa muislamu, miongoni mwa sadaka, au kumwacha huru mtumwa, au kuunganisha udugu, je katika mambo hayo kuna malipo? Basi akasema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-: " Umekwisha pokea malipo yako kutokana na mema uliyoyatanguliza".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaweka wazi Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa kafiri anaposilimu hulipwa kwa mema aliyokuwa akiyafanya kabla ya kusilimu miongoni mwa sadaka au kuacha huru mtumwa au kuunganisha udugu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kwa hakika mema aliyofanya kafiri hapa Duniani, hatolipwa kule Akhera, ikiwa atakufa akiwa kwenye ukafiri wake.