عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ المُؤْمنين رَضيَ اللهُ عنها قَالَتْ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُولُ:
«يُحْشَرُ النَّاسُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ حُفَاةً عُرَاةً غُرْلًا» قُلْتُ: يَا رَسُولَ اللهِ النِّسَاءُ وَالرِّجَالُ جَمِيعًا يَنْظُرُ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ؟ قَالَ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «يَا عَائِشَةُ، الْأَمْرُ أَشَدُّ مِنْ أَنْ يَنْظُرَ بَعْضُهُمْ إِلَى بَعْضٍ».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2859]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake- akisema:
"Watafufuliwa watu siku ya Kiyama wakiwa peku, uchi, hawajatahiriwa" Nikasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wanawake na wanaume wote pamoja, kila mmoja anamtazama mwenzake? Akasema rehema na amani ziwe juu yake: "Ewe Aisha, jambo litakuwa kubwa mno, kuliko hata mtu kushughulika kumtazama mwenzake".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2859]
Amesimulia Mtume rehema na amani ziwe juu yake baadhi ya yale yatakayokuwa siku ya Kiyama, na kwamba watakusanywa watu baada ya kufufuliwa kutoka makaburini mwao kwa ajili ya hesabu, na hali yao ni kwamba watakuwa miguu peku bila viatu, miili yao ikiwa uchi bila nguo wala kizuizi, na wakiwa hawajatahiriwa kama siku waliyozaliwa na mama zao, aliposikia mama wa Waumini Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake akasema kwa kustaajabu: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, wanawake na wanaume wote pamoja kila mmoja akimtazama mwenzake?! Mtume rehema na amani ziwe juu yake akambainishia: Kwa jambo la kisimamo na kukusanywa baada ya kufufuliwa kutoka katika kifo lina misukosuko kiasi kwamba watu macho yao hayatojali kutazama utupu.