+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه:
أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ كَانَ يَقُولُ فِي سُجُودِهِ: «اللهُمَّ اغْفِرْ لِي ذَنْبِي كُلَّهُ دِقَّهُ، وَجِلَّهُ، وَأَوَّلَهُ وَآخِرَهُ وَعَلَانِيَتَهُ وَسِرَّهُ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 483]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-:
Yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- alikuwa akisema katika sijida yake: "Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe mimi dhambi zangu ndogo zake na kubwa zake za mwanzo wake na mwisho wake, za wazi zake na za siri zake".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 483]

Ufafanuzi

Alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akiomba katika sijida yake akisema: "Ewe Mwenyezi Mungu nisamehe madhambi yangu" Kwa kuyasitiri, na unikinge na madhara yake; uyasamehe na usiyatazame na uyafute, "yote", nakusudia: "Za ndani" ndogo zake, na chache zake, "pana zake" kubwa zake na nyingi zake, "za mwanzo wake" dhambi ya kwanza, "na za mwisho zake", na zilizo kati yake, "za wazi zake na siri zake" miongoni mwa zile asizozijua yeyote ila wewe Uliyetakasika.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Amesema bin Qayyim: Na kuomba kusamehewa madhambi madogo na makubwa, ya ndani na ya juu, ya mwanzo na ya mwisho, ya siri na ya wazi, kukusanya huku na kueneza huku kwa sababu anataka ikija toba ije kwa yote anayoyajua mja miongoni mwa madhambi, na yale asiyoyajua.
  2. Imesemekana kuwa: Alitanguliza "Ya ndani" kabla ya " juu"; kwa sababu muombaji huanza na cha chini kisha anakwenda anapanda, yaani anapanda juu, kwa sababu madhambi makubwa mara nyingi hutokea kwa sababu ya kuendelea na madhambi madogo na kutojali, ni kana kwamba ni njia ya kuyaendea madhambi makubwa, na kinachokuwa ni sababu kina haki ya kutangulizwa kwa ajili ya kuthibitisha na kupandia kwenda juu.
  3. Kujinyenyekeza kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kumuomba msamaha kutokana na madhambi yote, madogo na makubwa.
  4. Amesema Nawawi: Hapa kuna msisitizo wa dua na kukithirisha matamshi yake hata kama baadhi yake yatatosheleza mengine.