عن أبي هريرة رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «إنه لَيَأتي الرَّجلُ السَّمين العظيم يوم القيامة لا يَزِنُ عند الله جَناح بَعُوضة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hakika atakuja mtu mnene tena mkubwa siku ya kiyama akiwa halingani mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hakika mtu mkubwa ni yule mwenye nia kubwa mwenye kujikweza kwa waja wa Mwenyezi Mungu duniani mwenye kujipa ujabari mwenye kujifaharisha kwa matendo yake na kauli zake, basi huyo siku ya kiyama hatolingana mbele ya Mwenyezi Mungu hata na uzito wa bawa la mbu, na wala hatokuwa na thamani wala nafasi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama