عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «لا يَستُرُ عبدٌ عبدًا في الدنيا إلا سَتَره الله يوم القيامة».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Hato msitiri mja mja mwenzie duniani isipokuwa atamsitiri Mwenyezi Mungu siku ya kiyama".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Muislamu atakapoona kwa ndugu yake maasi basi ni wajibu kwake ayasitiri na wala asiyasambaze kwa watu, kwani hilo ni katika kusambaza machafu, na atakayefanya hivyo kwa kutaraji radhi za Mwenyezi Mungu, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu atamlipa siku ya kiyama; kwa kumsitiri aibu zake na wala hatomfedhehesha mbele ya umati uliopo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama