عن جابر بن عبد الله رضي الله عنهما : أنه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم قبل موته بثلاثة أيام، يقول: «لا يَمُوتَنَّ أحدُكم إلا وهو يُحسنُ الظَّنَّ بالله عز وجل ».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Jabir bin Abdillahi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- yakwamba yeye alimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kabla ya kifo chake kwa siku tatu akisema: "Asife mmoja wenu isipokuwa naye awe na dhana nzuri na Mwenyezi Mungu Mtukufu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Jambo la wajibu kwa Muislamu aishi baina yakuwa na hofu na matumaini, hofu ya ghadhabu za Mwenyezi Mungu na hasira zake, na matumaini ya kupata msamaha wake na rehema zake, lakini wakati wa kuvuta hisia upande wa matumaini uzidi, na azidishe kumdhania vizuri Mwenyezi Mungu, na ataraji na ategemee rehema yake na msamaha wake, mpaka liwe hilo ni kizuizi cha yeye kukata tamaa na rehema za Mwenyezi Mungu kwa wakati huo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama