عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه مرفوعاً: «إنما الأعمال بِالنيَّات، وإنما لكل امرئ ما نوى، فمن كانت هجرتُه إلى الله ورسوله فهجرتُه إلى الله ورسوله، ومن كانت هجرتُه لدنيا يصيبها أو امرأةٍ ينكِحها فهجرته إلى ما هاجر إليه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Omari bin Khattwabi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika matendo yote huzingatiwa nia, na hakika kila mtu hulipwa kwa lile alilolinuia, atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi (malipo yake yatakuwa) ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya dunia au ataipata au kwaajili ya mwanamke ili amuoe, basi kuhama kwake kutakuwa ni kwa lile alilolihamia".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hadithi hii ina habari kubwa: Na wameichukulia baadhi ya wanachuoni kuwa ni theluthi ya uislamu, muumini analipwa kulingana na nia yake, na kulingana na kutengemaa kwake, yatakayekuwa matendo yake ni safi -yaani yamefanyika kwa ikhlaswi- basi yatakubalika hata kama yatakuwa kidogo na mepesi kwa sharti yaende sambamba na mfundisho ya Mtume rehema na Amani ziwe juu yake, na yatakayekuwa matendo yake ni kuwaonyesha watu na wala si safi kwaajili ya Mwenyezi Mungu basi hayo yatarudishwa hata kama ni makubwa na mengi. na kila amali iliyofanyika bila kutaka radhi za Mwenyezi Mungu, sawa sawa awe anayetafutwa ni mwanamke au mali au cheo au kinginecho katika mambo ya kidunia; basi hili linakuwa ni jibu kwa mfanyaji wake, kuwa hakubali Mwenyezi Mungu kutoka kwake, kwani sharti za kukubaliwa amali njema: ni iwe amali ni safi kwaajili ya Mwenyezi Mungu, na iwe imeafikiana na muongozo wa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhimizwa juu ya kutakasa nia, kwasababu Mwenyezi Mungu hakubali katika matendo ispokuwa yale yaliyokusudiwa kutafutwa ndani yake radhi zake.
  2. Matendo ambayo hujikurubisha watu kwayo kwa Mwenyezi Mungu -Aliyetakasika na kutukuka- atakapoyafanya mtu mzima kwa mfumo wa mazoea, haziambatani thawabu juu ya ufanyaji huo wa kawaida hata kama yatakuwa sahihi, mpaka akusudie kwayo kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.
  3. Fadhila za kuhama kwenda kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, nakuwa hilo ni katika matendo mema; kwasababu kitendo hicho hukusudiwa Mwenyezi Mungu.
  4. Hadithi hii ni moja ya hadithi ambazo uislamu mzima unazunguka juu yake, na kwasababu hiyo wamesema wanachuoni: Mzunguko mzima wa uislamu uko katika hadithi mbili: Nazo ni hii hadithi, na hadithi ya Aisha: "Atakayefanya jambo lolote ambalo siyo katika mafundisho yetu basi litarejeshwa" Hadithi hii ndiyo tegemezi la matendo ya moyo, na hii ndiyo kipimo cha matendo ya ndani, na hadithi ya Aisha: Ndiyo tegemezi la matendo ya viungo.
  5. Ni lazima kuzitofautisha ibada baadhi yake kwa baadhi, na ibada na miamala, nakuwa hakuna kinachotofautisha kati ya matendo yanayofanana katika namna ispokuwa nia.
  6. Amali yoyote ambayo haina kusudio lolote hiyo ni katika upuuzi, haina hukumu juu yake wala malipo.
  7. Atakayetakasa nia katika matendo yake atapata makusudio yake katika hukumu na malipo, na amali yake itakuwa ni sahihi, na yataambatana juu yake malipo, zitakapotimia sharti za matendo.
  8. Kuporomoka kwa matendo kwa kukosekana utakasifu wa nia kwaajili ya Mwenyezi Mungu.
  9. Kuidharau Dunia na matamanio yake kwa kauli yake: "Basi kuhama kwake kutakuwa ni kwa lile aliloliendea" Kiasi ambacho hakutaja anayoyapata mwenye kuhama kwaajili ya Dunia, tofauti na mwenye kuhama kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwani hapo yeye ameweka wazi yale yanayopatikana kwake, na hii ni katika ubainifu mzuri na ufasaha wa mazungumzo.