عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه مرفوعاً: «إنما الأعمال بِالنيَّات، وإنما لكل امرئ ما نوى، فمن كانت هجرتُه إلى الله ورسوله فهجرتُه إلى الله ورسوله، ومن كانت هجرتُه لدنيا يصيبها أو امرأةٍ ينكِحها فهجرته إلى ما هاجر إليه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Omari bin Khattwabi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika matendo yote huzingatiwa nia, na hakika kila mtu hulipwa kwa lile alilolinuia, atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi (malipo yake yatakuwa) ni kwaajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na atakayekuwa kuhama kwake ni kwaajili ya dunia au ataipata au kwaajili ya mwanamke ili amuoe, basi kuhama kwake kutakuwa ni kwa lile alilolihamia".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Hadithi hii ina habari kubwa: Na wameichukulia baadhi ya wanachuoni kuwa ni theluthi ya uislamu, muumini analipwa kulingana na nia yake, na kulingana na kutengemaa kwake, yatakayekuwa matendo yake ni safi -yaani yamefanyika kwa ikhlaswi- basi yatakubalika hata kama yatakuwa kidogo na mepesi kwa sharti yaende sambamba na mfundisho ya Mtume rehema na Amani ziwe juu yake, na yatakayekuwa matendo yake ni kuwaonyesha watu na wala si safi kwaajili ya Mwenyezi Mungu basi hayo yatarudishwa hata kama ni makubwa na mengi. na kila amali iliyofanyika bila kutaka radhi za Mwenyezi Mungu, sawa sawa awe anayetafutwa ni mwanamke au mali au cheo au kinginecho katika mambo ya kidunia; basi hili linakuwa ni jibu kwa mfanyaji wake, kuwa hakubali Mwenyezi Mungu kutoka kwake, kwani sharti za kukubaliwa amali njema: ni iwe amali ni safi kwaajili ya Mwenyezi Mungu, na iwe imeafikiana na muongozo wa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake.