عَنِ الزُّبَيْرِ بْنِ العَوَّامِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَأَنْ يَأْخُذَ أَحَدُكُمْ حَبْلَهُ، فَيَأْتِيَ بِحُزْمَةِ الحَطَبِ عَلَى ظَهْرِهِ، فَيَبِيعَهَا، فَيَكُفَّ اللَّهُ بِهَا وَجْهَهُ خَيْرٌ لَهُ مِنْ أَنْ يَسْأَلَ النَّاسَ أَعْطَوْهُ أَوْ مَنَعُوهُ».
[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 1471]
المزيــد ...
Kutoka kwa Zubair bin Awwam -radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Ikiwa mmoja wenu atachukua kamba yake, akaleta mzigo wa kuni juu ya mgongo wake, akauuza, na Mwenyezi Mungu akausitiri uso wake, basi hilo ni bora zaidi kwake kuliko kuwaomba watu wampe au wamnyime"
[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 1471]
Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mtu anapofanya kazi yoyote hata kama ni kuchukua kamba, akaitumia kukusanyia kuni juu ya mgongo wake, akaziuza na akapata chakula kwa hilo, au akatoa sadaka, na akajitosheleza na kutowaomba watu na akaulinda uso wake na udhalili wa kuombaomba; hilo ni bora zaidi kwake kuliko kuwaomba watu, ima wampe au wamnyime, kuwaomba watu ni udhalili, na muumini anaheshima na wala si dhalili.