عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضيَ اللهُ عنهُ سمعتُ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يقولُ:
«أَلاَ إِنَّ الدُّنْيَا مَلْعُونَةٌ، مَلْعُونٌ مَا فِيهَا، إِلاَّ ذِكْرُ اللهِ وَمَا وَالاَهُ وَعَالِمٌ أَوْ مُتَعَلِّمٌ».
[حسن] - [رواه الترمذي وابن ماجه] - [سنن الترمذي: 2322]
المزيــد ...
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Nilimsikia Mtume rehema na amani ziwe juu yake akisema:
"Tambueni kuwa dunia imelaaniwa, na vimelaaniwa vilivyomo, isipokuwa kumtaja Mwenyezi Mungu na yanayompendeza, na msomi, au mwanafunzi".
[Ni nzuri] - - [سنن الترمذي - 2322]
Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kwamba dunia na vilivyomo inachukiwa mbele ya Mwenyezi Mungu na haipendezi bali imetengwa mbali, yameachwa yote yaliyomo hayasifiki kwa uzuri; kwakuwa dunia na vilivyomo hushughulisha na kuwatenga mbali watu na Mwenyezi Mungu Mtukufu, isipokuwa kumtaja Mwenyezi Mungu na kila kinachokaribia hilo na kuwa katika aina hiyo katika yale anayoyapenda Mwenyezi Mungu, au mwalimu wa elimu ya kisheria anayewafundisha watu, au mwenye kujifunza.