عن ابن عمر رضي الله عنهما قال: سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: «يُدْنَى المؤمنُ يومَ القيامة من ربه حتى يضع كَنَفَهُ عليه، فيُقرِّرُه بذنوبِه، فيقول: أَتَعْرِفُ ذنبَ كذا؟ أَتَعْرِفُ ذنبَ كذا؟ فيقول: ربِّ أعرف، قال: فإني قد سَترتُها عليك في الدنيا، وأنا أغْفِرُها لك اليوم، فيعطى صحيفة حسناته».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Omari -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao-Amesema: Nilimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Atasogezwa muumini siku ya kiyama kwa Mola wake mpaka aweke upande wake kwake, kisha amtake akiri makosa yake, atasema: je unalifahamu dhambi fulani? atasema: Mola wangu nalijua, atasema basi mimi kwako nililisitiri duniani, na mimi ninalisamehe kwako leo hii, kisha atapewa kurasa za mema yake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Atamsogeza karibu Mwenyezi Mungu Mtukufu mja wake muumini siku ya kiyama, na amsitiri na watu waliosimama uwanjani, na amtake akiri makosa yake na maasi yake kwa siri, Je unalijua dhambi kadhaa?, atalikubali, atasema: basi hakika mimi nilikusitiri kwalo duniani na wala sikukufedhehesha nalo baina ya viumbe, na mimi vile vile nina lisitiri kwao leo hii, na ninalisamehe kwako.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama