عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: « يُسَلِّمُ الراكِبُ على الماشي، والماشي على القاعد، والقليلُ على الكثير».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Amsalimie aliyepanda anayetembea, na anayetembea aliyekaa, na wachache kwa wengi".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi hii: kumebainishwa kuwa ni nani mwenye haki zaidi ya kusalimiwa. Ya kwanza: Amsalimie aliyepanda anayetembea; kwasababu aliyepanda yuko juu, hivyo kuanza salamu toka upande wake ni dalili ya unyenyekevu wake kwa ndugu yake muislamu katika hali ya kujinyanyua kwake, likawa hilo linavuta zaidi mapenzi na upole kwake. Ya pili: Amsalimie anayetembea aliyekaa; kwa kufanana kwake na mwenye kuingia nyumbani, na hekima nyingine: nikuwa aliyekaa inaweza kuwa vigumu kuwachunga watu wote wenye kupita kwakuwa ni wengi: ukaondolewa ulazima wa kuanzia kwake kwa kumuondolewa tabu. Ya tatu: Ni wachache kuwasalimia wengi ikiwa ni ishara ya heshima na ukarimu kwa kikundi hiki. Ya nne: Nikuwa mdogo amsalimie mkubwa; kwasababu mkubwa ana haki kwa mdogo. lakini tukichukulia kuwa wachache wameghafilika na wakawa hawakusalimia basi wengi wao ndio wasalimie, na tukichukulia kuwa mdogo kajisahahu, akawa hakumsalimia mkubwa basi amsalimie na asiache sunna. Na hiki alichokitaja Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- haina maana kuwa mkubwa akimsalimia mdogo itakuwa haramu, lakini bora zaidi nikuwa: mdogo amsalimie mkubwa,basi asipomsalimia mkubwa ndio amsalimie, mkapa atakapofanya haraka kutoa salamu, kwa ushahidi uliotangulia katika hadithi ya umama: "Hakika mtu bora kwa Mwenyezi Mungu ni yule anayewaanza kwa salamu". Na hivyo hivyo lau ikitokea kukutana, basi mbora wao kwa Mwenyezi Mungu ni yule mwenye kuwaanza kwa salamu,na katika hadithi nyingine: "Na mbora wao ni yule anayeanza kwa salamu".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama