عَنِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ:
أَلَسْتُمْ فِي طَعَامٍ وَشَرَابٍ مَا شِئْتُمْ؟ لَقَدْ رَأَيْتُ نَبِيَّكُمْ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَمَا يَجِدُ مِنَ الدَّقَلِ مَا يَمْلَأُ بِهِ بَطْنَهُ.
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2977]
المزيــد ...
Kutoka kwa Nuuman bin Bashiri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema:
Hivi leo hii nyinyi si mnapata chakula na kinywaji mkitakacho? Kwa hakika mimi nilimuona Nabii wenu rehema na amani ziwe juu yake inafika mahala hapati hata tende mbovu ya kutosha kujaza tumbo lake.
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 2977]
Anaeleza Nuuman bin Bashiri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, maisha waliyonayo watu miongoni mwa neema, na kwamba wao muda wote wana uhakika wa chakula na kinywaji kwa kiwango watakacho, kisha akaeleza kuhusu hali ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake na kwamba alikuwa hapati katika tende mbovu kiasi cha kujaza tumbo lake kutokana na njaa.