عن البراء بن عازب رضي الله عنه مرفوعاً: «المسلمُ إذا سُئِلَ في القَبْرِ يَشْهَدُ أَنْ لا إلهَ إلا اللهُ، وأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللهِ، فذلك قولُهُ تعالى: (يُثَبِّتُ اللهُ الذِينَ آمَنُوا بالقَوْلِ الثَّابِتِ في الحَيَاةِ الدُّنْيَا وفي الآخِرَةِ) [إبراهيم: 27]».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Barraa bin Aazib -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Hadithi Marfu'u: "Muislamu atakapoulizwa kaburini anashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Hiyo ndiyo kauli yake Mtukufu: "Huwapa umakinifu Mwenyezi Mungu wale walioamani kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika akhera" [Ibrahim: 27].
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaulizwa muumini kaburini mwake, na wanamuuliza Malaika wawili mawakala wa hilo, nao ni Munkari na nakari, kama yalivyokuja majina yao katika sunani Tirmidhiy, akashuhudia kuwa hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu nakuwa Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Amesema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hii ndiyo kauli thabiti aliyoisema Mwenyezi Mungu ndani yake: "Huwapa umakinifu Mwenyezi Mungu wale walioamani kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika akhera" [Ibrahim: 27].

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama