عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من يُرِدِ الله به خيرا يُصِبْ مِنه».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie: "Mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri kwake humuonjesha".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anapotaka Mwenyezi Mungu kwa waja wake kheri basi huwapa mitihani katika nafsi zao na mali zao na watoto wao; ili liwe hilo ni sababu ya kufutiwa makosa yao na kunyanyuliwa daraja zao, na atakapozingatia mwenye akili mwisho wa matatizo hupata kuwa hilo ni kheri duniani na Akhera, na bila shaka kheri yake hasa huwa duniani; kwa yale yaliyomo miongoni mwa kurejea kwa Mwenyezi Mungu kwa dua na unyenyekevu na kudhihirisha kuhitaji, na ama marejeo ni miongoni mwa yale yaliyomo kama kufutiwa makosa na kunyanyuliwa daraja. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hakika tutakujaribuni kwa kitu katika hofu na njaa na kupungua katika mali na nafsi na matunda na wape habari njema wenye kusubiri", lakini hadithi hii iliyoachwa wazi inafungwa na hadithi nyingine ambayo inaonyesha kuwa makusudio ni: Yeyote mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri akasubiri na akataraji malipo, Mwenyezi Mungu akamuonjesha mpaka akampa mtihani, ama asipo subiri nikuwa mtu anaweza kupatwa na mitihani mingi na ikawa haina kheri ndani yake, na ikawa Mwenyezi Mungu hajamtakia kheri, makafiri hupatwa na mitihani mingi, pamoja na hilo wanabakia katika ukafiri wao mpaka wanakufanao, Hawa bila shaka hajawatakia kwao kheri.