عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من يُرِدِ الله به خيرا يُصِبْ مِنه».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie: "Mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri kwake humuonjesha".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Anapotaka Mwenyezi Mungu kwa waja wake kheri basi huwapa mitihani katika nafsi zao na mali zao na watoto wao; ili liwe hilo ni sababu ya kufutiwa makosa yao na kunyanyuliwa daraja zao, na atakapozingatia mwenye akili mwisho wa matatizo hupata kuwa hilo ni kheri duniani na Akhera, na bila shaka kheri yake hasa huwa duniani; kwa yale yaliyomo miongoni mwa kurejea kwa Mwenyezi Mungu kwa dua na unyenyekevu na kudhihirisha kuhitaji, na ama marejeo ni miongoni mwa yale yaliyomo kama kufutiwa makosa na kunyanyuliwa daraja. Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Na hakika tutakujaribuni kwa kitu katika hofu na njaa na kupungua katika mali na nafsi na matunda na wape habari njema wenye kusubiri", lakini hadithi hii iliyoachwa wazi inafungwa na hadithi nyingine ambayo inaonyesha kuwa makusudio ni: Yeyote mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri akasubiri na akataraji malipo, Mwenyezi Mungu akamuonjesha mpaka akampa mtihani, ama asipo subiri nikuwa mtu anaweza kupatwa na mitihani mingi na ikawa haina kheri ndani yake, na ikawa Mwenyezi Mungu hajamtakia kheri, makafiri hupatwa na mitihani mingi, pamoja na hilo wanabakia katika ukafiri wao mpaka wanakufanao, Hawa bila shaka hajawatakia kwao kheri.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa muumini nimwenye kupatwa na aina nyingi za balaa, sawa sawa iwe ni katika dini au mali.
  2. Habari njema na kubwa kwa muislamu, kwasababu kila muislamu haepukani nakuudhika.
  3. Mitihani inaweza kuwa ni alama ya Mwenyezi Mungu kumpenda mja wake, ili amnyanyue daraja yake, na kipande cheo chake, na afute makosa yake.