عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعاً: «من قام ليلة القَدْر إيمَانا واحْتِسَابًا غُفِر له ما تَقدم من ذَنْبِه».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Hadithi Marfu'u: "Atakaye simama usiku wenye cheo(Lailatul Qadri) kwa imani na kwa kutaraji malipo, atasamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hadithi imekuja kuzungumzia fadhila za kusimama usiku wenye cheo (Lailatul Qadri) na kuhimizwa juu ya hilo, kutakayeafikiana kusimama kwake na usiku wenye cheo, akiwa na imani nao na yale yaliyokuja katika fadhila zake na akitaraji kwa amali yake hiyo malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, hakusudii kwa hilo kujionyesha wala kutaka kusikika, wala kinginecho kinachokwenda kinyume na kutakasa nia na kutaraji malipo, basi hakika yatasamehewa yote madogo madogo katika madhambi yake, ama madhambi makubwa ni lazima alete toba ya kweli, ikiwa ni katika haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu, ama yakiwa yanaambatana na haki ya mwanadamu, la wajibu atubie kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na ajiweke mbali na haki ya mwenyenayo.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa usiku wenye cheo na kuhimizwa juu ya kuusimamisha.
  2. Nikuwa matendo mema hayasafishwi na wala hayakubaliki ispokuwa yanapokuwa pamoja na kutaraji malipo na nia za kweli.