+ -

عَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا:
أَنَّ رِجَالًا مِنْ أَصْحَابِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أُرُوا لَيْلَةَ القَدْرِ فِي المَنَامِ فِي السَّبْعِ الأَوَاخِرِ، فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «أَرَى رُؤْيَاكُمْ قَدْ تَوَاطَأَتْ فِي السَّبْعِ الأَوَاخِرِ، فَمَنْ كَانَ مُتَحَرِّيهَا فَلْيَتَحَرَّهَا فِي السَّبْعِ الأَوَاخِرِ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 2015]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Omari -radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-:
Yakwamba kuna baadhi ya watu katika Maswahaba wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, walionyeshwa Lailatul qadri ndotoni katika siku saba za mwisho wa Ramadhani. Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: "Naona ndoto zenu zimeafikiana katika siku saba za mwisho, basi atakayetaka kuitafuta basi na aitafute katika siku saba za mwisho".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 2015]

Ufafanuzi

Wanaume katika Maswahaba wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake waliona ndotoni kuwa Lailatul Qadri inakuwa katika siku saba za mwisho wa Ramadhani. Akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake: Ninaona ndoto zenu zimeafikiana katika siku saba za mwisho wa Ramadhani, atakayeitaka, akiwa na pupa ya kuitafuta, basi ajitahidi kuiwinda na kuitafuta kwa kukithirisha matendo mema kwani inatarajiwa zaidi kuwa katika siku saba za mwisho, nazo zinaanza kwanzia usiku wa tarehe ishirini na nne mwezi wa Ramadhani unapokuwa na siku thelathini, na zinaanza usiku wa tarehe thelathini na tatu mwezi unapokuwa wa siku ishirini na tisa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kireno Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa Lailatul-Qadri na himizo la kuitafuta.
  2. Miongoni mwa hekima za Mwenyezi Mungu na huruma yake aliuficha usiku huu ili watu waongeze juhudi katika ibada, kwa ajili ya kuutafuta, ili zikithiri thawabu zao.
  3. Usiku wa Lailatul-Qadri uko katika siku kumi za mwisho wa Ramadhani, na katika siku saba za mwisho ndio hutarajiwa zaidi.
  4. Usiku wenye cheo ni moja kati ya siku za kumi la mwisho la Ramadhani, nao ndio usiku ambao Mwenyezi Mungu aliiteremsha Qur'ani ndani yake kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, na akaufanya usiku huu kuwa ni bora kuliko miezi elfu moja katika baraka zake, na utukufu wa heshima yake, na athari ya matendo mema ndani yake.
  5. Umeitwa kuwa ni usiku wa Lailatul-Qadri, kwa kuiwekea sakna dali, ima ni kwa sababu ya utukufu wake, husemwa: Fulani anacheo kikubwa, inakuwa kuuambatanisha usiku ni katika sehemu ya kuambatanisha kitu katika sifa yake, yaani usiku mtukufu, yaani unacheo kikubwa kwa utukufu na thamani na nafasi mpaka mwisho wake, "Hakika sisi tumeiteremsha katika usiku wenye baraka" [Ad-Dukhan: 3]. Na ima imetokana na kukadiria: Inakuwa kuambatanishwa kwake ni kuambatanishwa kwa kiambata na kile kinachokizunguka, yaani ni usiku ambao ndani yake kunakuwa na makadirio ya yale yatakayoendelea katika mwaka mzima, "Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima" [Ad-Dukhan: 4].