عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «ما يزَال البَلاء بِالمُؤمن والمُؤمِنة في نفسه وولده وماله حتَّى يَلقَى الله تعالى وما عليه خَطِيئَة».
[حسن صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Halitoacha kumfika balaa muumini wa kiume na muumini wa kike katika nafsi yake na watoto wake na mali yake mpaka akutane na Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwa hana dhambi lolote".
Ni nzuri na nisahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Mwanadamu katika nyumba hii ya majukumu anakabiliwa na mitihani ya yenye kuumiza na yenye kufurahisha, pindi anapopatwa mwanadamu na balaa katika nafsi yake au watoto wake au mali yake, kisha akasubiri pale balaa linapoendelea, basi hilo linakuwa ni sababu katika kufutiwa madhambi pamoja na makosa, ama akilalamika basi mwenye kulalamika juu ya balaa basi hupata hasira za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama