عن أبي هريرة رضي الله عنه مرفوعًا: «مَن دَعَا إلى هُدى، كَان لَه مِنَ الأَجر مِثل أُجُور مَن تَبِعَه، لاَ يَنقُصُ ذلك مِن أُجُورِهِم شَيئًا، ومَنْ دَعَا إلى ضَلاَلَة، كان عَلَيه مِن الإِثْم مِثل آثَامِ مَن تَبِعَه، لاَ يَنقُصُ ذلك مِن آثَامِهِم شَيْئًا».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayelingania katika uongofu, atakuwa kwake kapata malipo mfano wa malipo ya aliyemfuata, halipunguzi hilo chochote katika malipo yao, na atakayelingania katika upotofu atakuwa kwake na madhambi mfano wa madhambi ya yule aliyemfuata, halipunguzi hilo katika madhambi yao chochote".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayelingania katika uongofu, atakuwa kwake kapata malipo mfano wa malipo ya aliyemfuata, halipunguzi hilo chochote katika malipo yao", atakayelingania katika uongofu: yaani: akaubainisha kwa watu na akawaita katika huo, mfano: akawabainishia watu kuwa rakaa mbili za dhuhaa ni sunna, nakwamba inampasa mtu aswali rakaa mbili za dhuha, kisha watu wakamfuata na wakaanza kuswali dhuha, basi atapata malipo mfano wa malipo yao bila kupungua katika malipo yao chochote; kwasababu fadhila za Mwenyezi Mungu ni pana. Au akawaambia watu kwa mfano: fanyeni mwisho wa swala zenu za usiku kuwa ni witiri, na wala msilale ila katika swala ya witiri isipokuwa atakayekusudia kusimama mwisho wa usiku basi aifanye witiri yake kuwa mwisho wa usiku, na watu wakamfuata katika hilo; basi atapata mfano wa malipo yao, yaani kila anaposwali witiri mmoja wao aliyemuongoza Mwenyezi Mungu kupitia yeye; anapata mfano wa malipo yake, na hivyo hivyo matendo mema yote yaliyobakia. Na katika kauli yake -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Atakayelingania katika upotofu atakuwa kwake na madhambi mfano wa madhambi ya yule aliyemfuata, halipunguzi hilo katika madhambi yao chochote", Yaani atakapowaita katika dhambi, na katika mambo ambayo ndani yake kuna madhambi, mfano akawaita watu katika mambo ya kipuuzi au ya batili au mziki au riba au mengineyo katika mambo ya haramu, basi hakika kila mtu aliyeathirika na maneno yake na yeye anaandikiwa mfano wa madhambi yao; kwasababu yeye ndiye aliyewaita katika mizigo hiyo ya madhambi. Kuwaita watu katika uongofu na kuwaita watu katika madhambi kunakuwa kwa kauli, kama akisema ninafanya kadhaa na ninafanya kadhaa, na kunakuwa kwa vitendo hasa hasa kwa wale ambao watu huwaiga (kama viongozi wa dini au wasanii na waigizaji na wacheza mpira) kwani atakapokuwa akiigwa kisha akafanya kitu inakuwa ni kana kwamba kawaita na wao kukifanya, na ndio maana wanachukua hoja ya yeye kukifanya kwake na wanasema mbona hata fulani alifanya kadhaa hii inafaa, kaacha kufanya kadhaa kumbe inafaa kuacha.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Thai Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama