عن عائشة رضي الله عنها قالت: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : "من أحدث في أمرنا هذا ما ليس منه فهو رد " وفي رواية " مَن عَمِلَ عملًا ليس عليه أمرُنا فهو رَدٌّ".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Atakayezua katika dini yetu hii yale yasiyokuwemo, basi yatarejeshwa" Na katika riwaya nyingine "Atakayefanya amali yoyote isiyokuwa ndani yake na maamrisho yetu, basi itarejeshwa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Kila amali au kauli ambayo haijaendana na sheria katika namna zake zote; kiasi kwamba haujaonyesha ushahidi wake na kanuni zake juu yake, basi hiyo itarejeshwa kwa mfanyaji wake wala haitokubalika kwake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Hukumu ya hakimu yoyote haibadilishi yaliyoko ndani ya amri ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, kwa kauli yake (Lisilokuwa katika maamrisho yetu) na makusudio yake ni dini.
  2. Dini kujengeka kwa misingi ya sheria.
  3. Uzushi wote wa kiitikadi na wa kimatendo ni batili, kama uzushi wa kupindisha- maana ya maneno ya Mwenyezi Mungu- na kutaraji-kheri bila kujituma- na kupinga makadirio ya Mwenyezi Mungu na kuwakufurisha watu kwasababu ya madhambi, na ibada zingine za kizushi.
  4. Nikuwa dini haiendi kwa rai na kwa kuangalia kama jambo ni zuri.
  5. Ni ishara ya ukamilifu wa dini.
  6. Kurudisha kila lililozushwa katika dini lisiloendana na sheria, na katika riwaya ya pili kumewekwa wazi kuacha kila uzushi sawa sawa ameuzusha mfanyaji wake au kaukuta.
  7. Kubatilishwa makubaliano na mikataba yote iliyokatazwa, na kutopatikana tija yake inayotakiwa.
  8. Katazo linamaanisha kutofaa jambo hilo, kwasababu yaliyokatazwa yote si katika jambo la dini hivyo ni wajibu kurudishwa.