+ -

عَنْ عَائِشَةَ رضي الله عنها قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم:
«مَنْ أَحْدَثَ فِي أَمْرِنَا هَذَا مَا لَيْسَ فِيهِ فَهُوَ رَدٌّ» متفق عليه. ولمسلم: «مَنْ عَمِلَ عَمَلًا لَيْسَ عَلَيْهِ أَمْرُنَا فَهُوَ رَدٌّ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 2697]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-:
"Atakayezua katika dini yetu hii, yale yasiyokuwemo, basi yatarejeshwa" Kaipokea Bukhari na Muslim. Na kutoka kwa Muslim: "Atakayefanya amali yoyote isiyokuwa na amri yetu, basi itarejeshwa".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 2697]

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa atakayetunga au kubuni jambo katika dini au akafanya amali yoyote ambayo haikuelekezwa na dalili yoyote kutoka katika Qur'ani na Sunna, basi jambo hilo litarejeshwa kwa mfanyaji wake na halitokubaliwa mbele ya Allah.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصربية الصومالية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية التشيكية Luqadda malgaashka Luqadda Oromaha Luqadda kinaadiga الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ibada zote zimejengeka juu ya yale yalikuja katika Qur'ani na Sunna, hatutakiwi kumuabudu Allah Mtukufu isipokuwa kwa sheria aliyoiweka na si kwa uzushi na mambo ya kutungwa.
  2. Dini haiendi kwa rai na kutazama lipi zuri, bali inakwenda kwa kumfuata Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake-.
  3. Hadithi hii ni ushahidi wa kukamilika dini.
  4. Uzushi ni kila kilichozushwa katika dini na hakikuwepo katika zama za Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- na Masahaba zake katika itikadi (Aqida) au kauli au amali yoyote.
  5. Hadithi hii ni msingi katika misingi ya Uislamu, nayo ni sawa na mzani kwa matendo, kama ambavyo kila amali ambayo haikukusudiwa kupata radhi za Allah Mtukufu, mfanyaji wake hana thawabu ndani yake, hivyo hivyo kila amali ambayo haitakuwa samabamba na yale aliyokuja nayo Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- basi hiyo itarejeshwa kwa mfanyaji wake.
  6. Uzushi uliokatazwa ni ule unaokuwa katika mambo ya dini na si ya kidunia.