عن مَسْلَمَةَ سَعِيدِ بْنِ يَزِيد قال: سألت أنس بن مالك: أكان النبي صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي في نَعْلَيْهِ؟ قال: «نعم».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Maslama Saidi bin Yazid amesema: nilimuuliza Anas bin Malik: alikuwa Nabii Rehema na Amani za Allah ziwe juu yake- akiswali na viatu vyake? akasema: ((ndio)).
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Katika madhumuni ya sheria ni kutofautiana na watu wa kitabu, (Mayahudi na wakristo), nakuondoa kila kitu ambacho ndani yake kina tabu na uzito juu ya muislamu, na alimuuliza Saidi bin thabit naye ni katika waaminifu wakubwa miongoni mwa wanafunzi wa maswahaba, kamuuliza Anas bin Maliki -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuhusu Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Hivi je alikuwa akiswali na viatu vyake; ili iwe kwake ni kiigizo? Au ni kwasababu aliliona hilo haliwezekani kwasababu yakuwa mara nyingi huwa na uchafu na udhia, Anasi akamjibu, Ndiyo, alikuwa akiswali na viatu vyake, nakuwa hilo ni katika sunna zake takatifu, na hili si maalumu kwa ardhi fulani au zama maalumu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama