+ -

عَنْ بُسْرِ بْنِ سَعِيدٍ، أَنَّ زَيْدَ بْنَ خَالِدٍ الْجُهَنِيَّ رَضيَ اللهُ عنه، أَرْسَلَهُ إِلَى أَبِي جُهَيْمٍ رَضيَ اللهُ عنه، يَسْأَلُهُ مَاذَا سَمِعَ مِنْ رَسُولِ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي الْمَارِّ بَيْنَ يَدَيِ الْمُصَلِّي؟ قَالَ أَبُو جُهَيْمٍ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«لَوْ يَعْلَمُ الْمَارُّ بَيْنَ يَدَيِ الْمُصَلِّي مَاذَا عَلَيْهِ لَكَانَ أَنْ يَقِفَ أَرْبَعِينَ خَيْرًا لَهُ مِنْ أَنْ يَمُرَّ بَيْنَ يَدَيْهِ» قَالَ أَبُو النَّضْرِ: لَا أَدْرِي قَالَ: أَرْبَعِينَ يَوْمًا أَوْ شَهْرًا أَوْ سَنَةً؟

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 507]
المزيــد ...

Kutoka kwa Busru bin Saidi, ya kwamba Zaidi bin Khalidi Al-Juhani, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alimtuma kwenda kwa Abuu Juhaim radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amuulize alisikia nini kutoka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu mtu anayepita mbele ya anayeswali? Akasema Abuu Juhaim: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Lau angejua mwenye kupita mbele ya mwenye kuswali nini anachokipata, basi kusimama arobaini ni bora kwake kuliko kupita mbele yake" Amesema Abuu Nasri: Sijui alisema: Siku arobaini au miezi au miaka?

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 507]

Ufafanuzi

Alitahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kupita mbele ya mwenye kuswali swala ya faradhi au sunna, na kwamba lau angelijua mwenye kufanya hivyo kwa makusudi yale anayoyapata katika madhambi; basi angechagua kusimama arobaini; hilo ni bora zaidi kwake kuliko kupita mbele yake. Amesema Abuu Nasri mpokezi wa hadithi: Sijui alisema: Siku arobaini, au miezi au miaka.

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kupita mbele ya mwenye kuswali, atakapokuwa hana kizuizi (sutra), au kupita kati yake na kizuizi atakapokuwa na kizuizi.
  2. Amesema bin Hajari: Na wakatofautiana wanachuoni katika kuweka kiwango cha hilo pakasemwa: Atakapopita kati yake na kiasi cha kusujudu kwake, na pakasemwa: Kati yake yeye na huyo kuwe na futi tatu, na pakasema: kuwe kati yake na yeye kiwango cha kurusha jiwe.
  3. Amesema Suyutwi: Makusudio ya kupita ni apite mbele yake kwa makusudi, ama akipita mbele yake akiwa anakwenda upande wa kibla hii haiingii katika ahadi hiyo ya adhabu.
  4. Kilicho bora nikuwa mwenye kuswali asiswali katika njia za watu, na katika sehemu ambazo hawana budi lazima wapite, ili asiitie swala yake katika mapungufu, na asiwatie katika makosa wenye kupita, na anatakiwa aweke kizuizi kitakachozuia kati yake na wenye kupita.
  5. Inachukuliwa katika hadithi hii kuwa; madhambi yoyote yanayohusu maasi Akhera hata kama ni kidogo basi ni makubwa mno kuliko shida yoyote ya duniani, vyovyote vile itakavyokuwa shida hiyo.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama