عن عائِشَة رضي الله عنها مرفوعاً: «لا صلاة بِحَضرَة طَعَام، وَلا وهو يُدَافِعُه الأَخبَثَان».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi marfu'u: "Hakuna swala chakula kikiwa tayari, na hakuna swala kwa mwenye kuhisi haja kubwa na ndogo"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Inatia mkazo hadithi hii, matakwa ya sheria katika kuhudhuria moyo wa mtu mzima katika swala mbele ya Mola wake, na haliwi hilo ila kwa kuyakata yote yanayoweza kumshughulisha; ambayo yakiwepo yanasababisha kukosekana kwa utulivu na unyenyekevu; kwaajili hii: bila shaka sheria imekataza kuswali wakati chakula kinapotengwa ambacho kitaitamanisha nafsi ya mwenye kuswali, na moyo wake utafungamana nacho, na vile vile inakataza kuswali kukiwa na kuvizuia vichafu viwili (Haja kubwa na ndogo) Ambavyo ni mkojo na kinyesi; asishughulishe fikra zake na kuzuia udhia.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Machukizo ya kuswali katika hali ya kuzuia vichafu viwili, pale ambapo muda hautokuwa mfinyu swala ikampita, na akiswali naye akiwa katika hali hiyo swala yake ni sahihi lakini inamapungufu haijakamilika, kwa mujibu wa hadithi iliyotajwa na haina haja ya kuirudia, na ama akiingia katika swala hali yakuwa havisukumi vichafu viwili, bali limejitokeza hilo wakati wa swala hapo swala yake ni sahihi wala hakuna machukizo ndani yake endapo tu hakutomzuia huku kupambana navyo kumalizia swala.
  2. Kuhudhuria moyo na unyenyekevu ni mambo yanayotakiwa katika swala.
  3. Inamlazimu mwenye kuswali kuviweka mbali vyote vinavyo mshughulisha katika swala yake.
  4. Kubanwa haja ndogo au haja kubwa huo ni udhuru wa kuacha ijumaa na jamaa, kwa sharti asifanye nyakati za swala ndio muda wa kubanwa.