عن عائِشَة رضي الله عنها مرفوعاً: «لا صلاة بِحَضرَة طَعَام، وَلا وهو يُدَافِعُه الأَخبَثَان».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi marfu'u: "Hakuna swala chakula kikiwa tayari, na hakuna swala kwa mwenye kuhisi haja kubwa na ndogo"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Inatia mkazo hadithi hii, matakwa ya sheria katika kuhudhuria moyo wa mtu mzima katika swala mbele ya Mola wake, na haliwi hilo ila kwa kuyakata yote yanayoweza kumshughulisha; ambayo yakiwepo yanasababisha kukosekana kwa utulivu na unyenyekevu; kwaajili hii: bila shaka sheria imekataza kuswali wakati chakula kinapotengwa ambacho kitaitamanisha nafsi ya mwenye kuswali, na moyo wake utafungamana nacho, na vile vile inakataza kuswali kukiwa na kuvizuia vichafu viwili (Haja kubwa na ndogo) Ambavyo ni mkojo na kinyesi; asishughulishe fikra zake na kuzuia udhia.