عَن أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَا بَالُ أَقْوَامٍ يَرْفَعُونَ أَبْصَارَهُمْ إِلَى السَّمَاءِ فِي صَلاَتِهِمْ»، فَاشْتَدَّ قَوْلُهُ فِي ذَلِكَ، حَتَّى قَالَ: «لَيَنْتَهُنَّ عَنْ ذَلِكَ أَوْ لَتُخْطَفَنَّ أَبْصَارُهُمْ».
[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 750]
المزيــد ...
Imepokelewa kutoka kwa Anasi bin Maliki -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Hivi wana nini watu! wananyanyua macho yao mbinguni ndani ya swala zao", ikazidi ukali kauli yake katika hilo, mpaka akasema: "Hakika, ni ima waache kufanya hivyo, au yatapofuliwa macho yao".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 750]
Aliwatahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake wale wanaonyanyua macho yao mbinguni ndani ya swala wakati wa dua au kinginecho, kisha karipio lake likawa kali na akatangaza adhabu rehema na amani ziwe juu yake kwa wanaofanya hivyo kwamba yanahofiwa macho yao kupofuliwa na yakanyakuliwa kwa haraka kwa namna wasiyoitarajia, wakajikuta tayari wamepoteza neema ya macho.