عن عائشة - رضي الله عنها-، أن أمَّ سَلَمَة، ذَكَرَت لرسول الله صلى الله عليه وسلم كَنِيسة رأتْهَا بأرض الحَبَشَةِ يُقال لها مَارِيَة، فذَكَرت له ما رأَت فيها من الصُّور، فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «أولئِكِ قوم إذا مات فيهم العَبد الصالح، أو الرُّجل الصَّالح، بَنُوا على قَبره مسجدا، وصَوَّرُوا فيه تلك الصِّور، أولئِكِ شِرَار الخَلْق عند الله».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha Radhi za Allah ziwe juu yake: "ya kwamba Ummu Salama alimueleza Mtume Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake kanisa aliloliona Ethiopia linaloitwa Maria, Akamsimulia aliyoyaona ndani yake miongoni mwa mapicha, akasema Mtume Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake: "Hao ni watu ambao anapokufa kwao mja mwema, au mtu mwema, wanajenga juu ya kaburi lake msikiti, na wanachora hapo mapicha, hao ni viumbe waovu mbele ya Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anaeleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Ummu salama- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- alipokuwa katika Ardhi ya Ethiopia aliona kanisa ndani ya kuna mapicha, Akamsimulia Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- alichokiona ndani yake miongoni mwa kupambwa vizuri kwa mapicha; kwa kulishangaa hilo, na kwasababu ya kulikuza hili na hatari yake juu ya Tauhidi; Alinyanyua Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kichwa chake, na akawabainishia sababu za kuweka mapicha haya; kwa kuutahadharisha umma wake juu ya yale waliyoyafanya hao, Na akasema: hakika hao unaowataja walikuwa anapokufa kwao mtu mwema wanajenga juu ya kaburi lake msikiti na wanaswali ndani yake, na wanachora picha hizo, na akabainisha kuwa mwenye kufanya hivyo ni kiumbe muovu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu-; kwasababu kitendo hicho kinapelekea katika kumshirikisha Mwenyezi Mungu -Mtukufu-.