عن عائشة - رضي الله عنها-، أن أمَّ سَلَمَة، ذَكَرَت لرسول الله صلى الله عليه وسلم كَنِيسة رأتْهَا بأرض الحَبَشَةِ يُقال لها مَارِيَة، فذَكَرت له ما رأَت فيها من الصُّور، فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «أولئِكِ قوم إذا مات فيهم العَبد الصالح، أو الرُّجل الصَّالح، بَنُوا على قَبره مسجدا، وصَوَّرُوا فيه تلك الصِّور، أولئِكِ شِرَار الخَلْق عند الله».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha Radhi za Allah ziwe juu yake: "ya kwamba Ummu Salama alimueleza Mtume Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake kanisa aliloliona Ethiopia linaloitwa Maria, Akamsimulia aliyoyaona ndani yake miongoni mwa mapicha, akasema Mtume Rehma na Amani za Allah ziwe juu yake: "Hao ni watu ambao anapokufa kwao mja mwema, au mtu mwema, wanajenga juu ya kaburi lake msikiti, na wanachora hapo mapicha, hao ni viumbe waovu mbele ya Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anaeleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Yakwamba Ummu salama- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- alipokuwa katika Ardhi ya Ethiopia aliona kanisa ndani ya kuna mapicha, Akamsimulia Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- alichokiona ndani yake miongoni mwa kupambwa vizuri kwa mapicha; kwa kulishangaa hilo, na kwasababu ya kulikuza hili na hatari yake juu ya Tauhidi; Alinyanyua Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kichwa chake, na akawabainishia sababu za kuweka mapicha haya; kwa kuutahadharisha umma wake juu ya yale waliyoyafanya hao, Na akasema: hakika hao unaowataja walikuwa anapokufa kwao mtu mwema wanajenga juu ya kaburi lake msikiti na wanaswali ndani yake, na wanachora picha hizo, na akabainisha kuwa mwenye kufanya hivyo ni kiumbe muovu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu-; kwasababu kitendo hicho kinapelekea katika kumshirikisha Mwenyezi Mungu -Mtukufu-.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kujenga misikiti juu ya makaburi, au kuzika wafu msikitini; kwaajili ya kuziba njia za ushirikina na kujiweka mbali na kujifananisha na waabudu masanamu.
  2. Nikuwa kujenga misikiti juu ya makaburi, na kusimika picha katika msikiti hiyo ni kazi ya mayahudi na wakristo, nakuwa atakayefanya hivi basi atakuwa kafanana nao na atakuwa kastahiki adhabu wanayostahiki.
  3. Nikuwa kuswali katika kaburi ni njia inayopelekea katika ushirikina, sawa sawa kaburi liwe ndani ya msikiti au nje.
  4. Uharamu wa kuwa na picha zitakapokuwa ni za viumbe vyenye roho.
  5. Nikuwa atakayejenga juu ya kaburi msikiti na akachora ndani yake picha, huyo ni muovu zaidi katika viumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  6. Ulinzi wa sheria upande wa tauhidi ni ulinzi uliokamilika; kiasi ambacho imeziba njia zote ambazo zinaweza kupelekea katika ushirikina.
  7. Kutokubalika swala katika msikiti uliojengwa juu ya kaburi; kwasababu Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake amekataza hilo na akamlaani mfanyaji wake, na katazo linamaanisha kuharibika kwa kile kilichokatazwa.
  8. Pupa ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- juu ya kuuongoza umma wake; amelielekeza hilo Rehema na Amani ziwe juu yake- naye akiwa katika kitanda cha mauti yake anautahadharisha umma wake kutokana na kitendo cha mayahudi na wakristo kwa Manabii wao na wema wao.
Ziada