عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «لا نِكاح إلا بِوَلِيّ».
[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وابن ماجه والدارمي وأحمد]
المزيــد ...

kutoka kwa Abii Musa Al-Ash'ariy radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Mtume rehema na Amani zimfikie, amesema: "Hakuna ndoa bila walii (msimamizi)".
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Imeonyesha hadithi juu ya kumzingatia walii katika kufunga ndoa nakuwa hilo ni sharti la kusihi kwake, hivyo haikubaliki ndoa ila kwa walii, anayesimamia ufungishaji wa ndoa, na ni sharti kwa walii: Utuuzima (kubalehe), na kuwa mwanaume, na uelevu katika kujua maslahi ya ndoa, na kuwiana katika dini (kuwa katika dini moja) kati ya msimamizi na msimamiwa, ambaye hatosifika kwa sifa hizi, basi atakuwa hastahiki kusimamia kufungisha ndoa, ikishindikana basi msimamizi wake atakuwa kiongozi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kupatikana kwa msimamizi ni sharti katika kusihi ndoa.
  2. walii ni mwanaume wa karibu kwa mwanamke, asimuozeshe walii wa mbali katika ukoo hali yakuwa kuna wa karibu yake.
  3. kuharibika kwa ndoa isiyo na walii, na inazingatiwa kuwa ni ndoa isiyokuwa ya kisheria, na ni wajibu kuivunja kwa hakimu au kwa talaka ya kisheria.
  4. Asipopatikana walii kwa mwanamke katika ndugu zake wa karibu, au wa upande wa baba yake, basi msimamizi wake ni imamu au naibu wake, kwasababu mwenye mamlaka ni msimamizi kwa asiyekuwa na msimamizi.
  5. Ni lazima msimamizi awe ni muelevu, kwasababu hayawezi kutimia maslahi kwa mwanamke, ispokuwa atakapokuwa msimamizi ni muelevu.