+ -

عن أبي موسى رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال:
«لا نِكَاحَ إِلّا بِوَليٍّ».

[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وابن ماجه وأحمد] - [سنن أبي داود: 2085]
المزيــد ...

Na kutoka kwa Abuu Musa Radhi za Allah ziwe juu yake- yakuwa Mtume Rehema na amani za Allah ziwe juu yake amesema:
"Hakuna ndoa ila kuwe na walii (Msimamizi)".

Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa mwanamke haikubaliki ndoa yake ila kwa walii atakayesimamia kufungwa kwa ndoa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية القيرقيزية النيبالية اليوروبا الليتوانية الدرية الصومالية الكينياروندا التشيكية المالاجاشية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Walii ni sharti la kusihi ndoa, ikifanyika bila walii, au mwanamke akajiozesha mwenyewe, haikubaliki.
  2. Walii ni ndugu wa karibu wa kiume kwa mwanamke, asiozeshwe na walii wa mbali akiwepo walii wa karibu yake.
  3. Ni sharti kwa walii: Awe mtu mzima (Aliyebalehe), mwanaume, na uwezo wa kupambanua na kujua masilahi ya ndoa, na wawe katika dini moja, msimamizi na msimamiwa, asiyekuwa na sifa hizi hastahiki kuwa msimamizi wa kufungisha ndoa.