عن عبد الله بن مسعود رضي الله عنه قال: علمنا رسول الله صلى الله عليه وسلم خطبة الحاجة: إن الحمد لله، نستعينه ونستغفره، ونعوذ به من شرور أنفسنا، من يهد الله، فلا مضل له، ومن يضلل، فلا هادي له، وأشهد أن لا إله إلا الله، وأشهد أن محمدا عبده ورسوله، " يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُمْ مِنْ نَفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالًا كَثِيرًا وَنِسَاءً وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ والأرحام إن الله كان عليكم رقيبا} [النساء: 1] ، {يا أيها الذين آمنوا اتقوا الله حق تقاته ولا تموتن إلا وأنتم مسلمون} [آل عمران: 102] ، {يا أيها الذين آمنوا اتقوا الله وقولوا قولا سديدا (70) يصلح لكم أعمالكم ويغفر لكم ذنوبكم ومن يطع الله ورسوله فقد فاز فوزا عظيما} [الأحزاب:70 - 71].
[صحيح] - [رواه أبو داود والترمذي وابن ماجه والنسائي وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillahi bin Mas'udi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: Alitufundisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Hotuba ya haja: Hakika kila sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, tunamtaka msaada na tunamuomba msamaha, na tunajilinda kwake kutokana na shari ya nafsi zetu, mwenye kumuongoza Mwenyezi Mungu, hakuna wa kumpoteza, ana anayempoteza, hakuna wa kumuongoza, na nina shuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, na ninashuhudia kuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake, "Enyi watu, mcheni Mola wenu aliyekuumbeni kutokana na nafsi moja, na akaumba kutokana na nafsi hiyo mwanamke, na akatoa kutokana na nafsi hiyo wanaume na wanawake wengi, na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwake mnaombana na jamaa zenu, hakika Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi ni mlinzi" [An nisaa: 1], "Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu ukweli wa kumcha na wala msife ila na nyinyi ni waislamu" [Al Imran: 102], "Enyi mlioamini mcheni Mwenyezi Mungu na mseme kauli ya sawa [70] akutengenezeeni amali zenu na akusameheni madhambi yenu na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake basi atakuwa kafaulu kufaulu kukubwa" [Al Ahzaab: 70-71].
Sahihi - Imepokelewa na Ibnu Maajah
Imeonyesha hadithi ya bin Mas'udi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, juu ya sheria ya hotuba hii iliyokusanya sifa nyingi za Mwenyezi Mungu, na kutaka msaada wake, na kujilinda kwake kutokana na shari, na kusoma aya zile tukufu, na inampasa mtu azitangulize mbele wakati wa kuzungumza na watu katika elimu, hiyo ni katika mafundisho ya kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna, na utambuzi wa sheria, na mawaidha kwa watu, haihusu ndoa pekee, bali ni hotuba ya kila haja; ili ziteremke baraka, na kuwe na athari nzuri katika yale unayoyatoa, hiyo ni sunna iliyotiliwa mkazo.