عَنْ عُقْبَةَ بْنَ عَامِرٍ الْجُهَنِيَّ رضي الله عنه قَالَ:
ثَلَاثُ سَاعَاتٍ كَانَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَنْهَانَا أَنْ نُصَلِّيَ فِيهِنَّ، أَوْ أَنْ نَقْبُرَ فِيهِنَّ مَوْتَانَا: حِينَ تَطْلُعُ الشَّمْسُ بَازِغَةً حَتَّى تَرْتَفِعَ، وَحِينَ يَقُومُ قَائِمُ الظَّهِيرَةِ حَتَّى تَمِيلَ الشَّمْسُ، وَحِينَ تَضَيَّفُ الشَّمْسُ لِلْغُرُوبِ حَتَّى تَغْرُبَ.
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 831]
المزيــد ...
Kutoka kwa Ukba bin Aamir Al-Juhani radhi za Allah ziwe juu yake amesema:
Nyakati tatu alikuwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake akitukataza kuswali ndani yake, au kuzika ndani yake maiti wetu: wakati linapoanza kuchomoza jua mpaka linyanyuke, na wakati linapofika kati kati mpaka lipinde, na wakati linapoanza kuzama mpaka lizame.
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim] - [صحيح مسلم - 831]
Amekataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake nyakati tatu za mchana kutoswali ndani yake swala za sunna, au kuzikwa ndani yake maiti: Wakati wa kwanza: Wakati linapodhihiri jua kwa kuchomoza, na hii ni wakati wa mwanzo wa kuchomoza kwake mpaka linyanyuke kiasi cha mkuki, na inakadiriwa kuwani robo saa takribani. Wakati wa pili: Pindi jua linapofika kati kati ya mbingu, linapokuwa halina kivuli upande wa Mashariki au Magharibi mpaka linapoondoka kutoka kati kati ya mbingu, na kikaonekena kivuli upande wa Mashariki, wakati ambapo unaanza wakati wa Adhuhuri, nao ni wakati mfupi mno; ambao ni kiasi cha dakika tano takribani. Wakati wa tatu: Linapopinda na likaanza kuzamia Magharibi mpaka lizame.